Saturday, October 31, 2015

MAGUFULI AWASHUKURU WAPIGA KURA

 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wapenzi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi waliojitokeza kwa wingi kwenye hafla fupi ya kumpongeza Dk. John Pombe Magufuli kwa ushindi alioupata katika uchaguzi wa uliofanyika oktoba 25 mwaka 2015. 
 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia)akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahma Kinana(katikati) pamoja na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda wakati wa sherehe ndogo ya kushukuru wapiga kura walioipa CCM ushindi.
 Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akiwashukuru wananchi wote waliompigia kura kwenye uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 25, oktoba ambapo aliibuka mshindi katika uchaguzi huo.
 Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akiwashukuru wananchi wote
waliompigia kura kwenye uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 25, oktoba
ambapo aliibuka mshindi katika uchaguzi huo.
 Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo kwa  wananchi waliojitokeza kumpongeza nje ya Makao Makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba.
Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akionyesha cheti alichokabidhiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mara baada ya kushinda kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka 2015.
 Mama Samia Suluhu aliyekuwa Mgombea Mwenza akionyesha cheti chake cha Umakamu wa Rais kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliokuja kumpongeza.
 Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akimtambulisha mke wake Janeth Magufuli mbele ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliokuja kumpongeza.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Rais mteule wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza kwenye hafla hiyo ya kumpongeza Dk. John Pombe Magufuli nje ya Ofisi Ndogo CCM Lumumba.
 Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akiwaaga wakazi wa jiji la Dar es Salaam mara baada ya kumalizika hafla ya kuwasalimu na kuwashukuru kwa kumpigia kura zilizompa ushindi wa kiti cha Urais.
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kumpongeza Dk. John Pombe Magufuli nje ya ofisi ndogo CCM Lumumba. BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KIWIA AKANUSHA KUZIMIA BAADA YA MATOKEO KUTANGAZWA. ASEMA ANATARAJIA KUFUNGUA KESI MAHAKAMANI KWANI BADO HAJASAINI MATOKEO.

Highness Kiwia akionyesha moja ya karatasi yenye makosa
Na:George Binagi-GB Pazzo
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi Ukawa Highness Kiwia, anatarajia kufungua kesia ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimboni humo kwa madai kwamba haukuwa wa huru na haki kutokana na kugubikwa na changamoto mbalimbali.

Kiwia ambae ameshindwa kutetea jimbo hilo baada kuchukuliwa na Angelina Mabula kutoka Chama cha Mapinduzi CCM, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na Uchaguzi huo.

Alieleza kuwa katika vituo mbalimbali jimboni humo kulikuwa na makosa mengi ambayo ni pamoja na uwepo wa vituo hewa, idadi ya wapiga kura kutofautiana na idadi ya waliojiandikisha katika daftari la kupigia kura pamoja na majina ya wapiga kura kukutwa katika majimbo tofauti na yale waliyojiandikishia.

Katika hatua nyingine Kiwia alikanusha taarifa kuwa alimtuma mwakilishi kwa ajili ya kusaini fomu ya matokeo kwa niaba yake na kwamba siku ya kutangaza matokeo alishindwa kupokea matokeo hayo na hivyo kuzilai.

Kwa upande wake Tungaraza Njugu ambae ni Kiongozi wa Kanda ya Ziwa Victoria Chadema, alisema kuwa zoezi la uchaguzi mwaka huu linapaswa kulaaniwa kwa kuwa halikuendeshwa kidemokrasia kutokana na kukiuka taratibu mbalimbali za uchaguzi.

Katika Matokeo ya Kiti cha Ubunge Jimboni Ilemela, Mgombea wa CCM Angelina Mabula aliibuka mshindi baada ya kupata kura 85,424 na kufuatiwa na mgombea wa Chadema Highness Kiwia aliepata kura 61,679 ambapo kwa upande wa Madiwani CCM ilishinda Kata 16 huku Kata Tatu zikichukuliwa na upinzani.
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA

Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chadema
Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chadema akiongea na wanahabari
Kiwia akiteta jambo katika Mkutano na Wanahabari
Kutoka Kushoto ni Humphrey Mhada ambae ni Mwenyekiti Kanda ya Ziwa Victoria Chadema, Highness Kiwia ambae alikuwa mgombea Jimbo la Ilemela Chadema na Hassan Haji ambae alikuwa Meneja Kampeni Jimboni Ilemela
Press Conference
Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chadema akiongea na wanahabari
Wa kwanza kulia waliokaa ni Tungaraza Njugu ambae ni Kiongozi wa Kanda ya Ziwa Victoria Chadema akiongea katika mkutano na wanahabari
Peter Kaiza ambae alikuwa Mgombea Udiwani Kata ya Ibungilo Ilemela akionyesha moja ya karatasi yenye makosa
Kutoka Kushoto ni Julius Malifedha ambae ni Katibu Mwenezi Chadema Ilemela, Peter Kaiza aliekuwa Mgombea Udiwani Kata ya Ibungilo na Ivonne Highness ambae alikuwa Mratibu wa Kampeni za Uchaguzi
Kada wa Chama
BINAGI MEDIA GROUP, KWA PAMOJA TUJUZE JAMII

LINI MAGUFULI ATATEUA MAWAZIRI? MAGUFULI AWAPASHA WANAFIKI, HALI TETE ZANZIBAR MAGAZETI YA LEO.

Magufuli awapasha wanafiki, Vijana wa UKAWA waachiwa kwa dhamana, Tume ya uchaguzi yamaliza kazi rasmi. Pitia dondoo za magazeti;

GAZETI LA MWANANCHI
SATURDAY, OCTOBER 31, 2015

Kaa chonjo, saa mbaya




Rais Mteule Dk John Magufuli
Rais Mteule Dk John Magufuli 
By Julius Mathias na Beatrice Moses, MWANANCHI
Dar es Salaam. Ni kama alikuwa akisema “kaa chonjo, saa mbaya” wakati Rais Mteule Dk John Magufuli alipohutubia kwa mara ya kwanza tangu atangazwe kuwa mshindi wa mbio za urais.
Dk Magufuli, ambaye alikuwa akihutubia wafuasi wa CCM nje ya ofisi ndogo za chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi wa urais, alituma salamu hizo kwa watendaji serikalini na hata kwa wanachama wa CCM aliowaita wanafiki.
Waziri huyo wa zamani wa Ujenzi aliwataka watendaji wa Serikali wanaotumia ofisi za umma kama vijiwe; kwa manufaa yao binafsi; wasiojali wananchi; na wanaofanya kazi kwa mazoea, kujiandaa kuondoka.
“Rais wangu, mwenyekiti wangu Jakaya Kikwete utanisamehe kwa hatua nitakazozichukua kwa watu uliowalea wakati wa utumishi wako, na hawa ndiyo waliokukwamisha,” alisema Dk Magufuli ambaye alikuwa akijinasibu kwa uchapakazi wakati wa kampeni zake.
“Watu wanafanya kazi kwa mazoea. Wengine hawajali kabisa mahitaji ya wananchi wanaofika kwenye ofisi wanavyotaka. Utanisamehe Rais wangu, hawa ndiyo waliochangia kukukwamisha. Kwenye Serikali yangu wajiandae kuondoka.”
Dk Magufuli alikuwa akiwashukuru wanachama na wafuasi wa CCM muda mfupi baada ya kukabidhiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) cheti cha ushindi katika uchaguzi wa Rais kwenye hafla iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee. Wakati hali ya kisiasa Zanzibar ikiwa tete, hakukuwapo na viongozi wengi kutoka visiwa hivyo, zaidi ya Samia Suluhu Hassa, ambaye ni Makamu Mteule wa Rais.
Dk Magufuli alisema amezunguka nchi yote na kukutana na wananchi ambao wamemueleza kero mbalimbali.
“Nimegundua wengi wana matumaini makubwa sana na mimi. Binafsi, ninauona ugumu wa kazi iliyo mbele yangu, lakini nitaifanya na nafahamu kuwa nitagusa maslahi ya wengi, hivyo wajiandae,” alisema Dk Magufuli, ambaye ameibuka na ushindi wa kura 8,882,935, ikiwa ni tofauti ya zaidi ya kura milioni 2.8.
Akiwa jukwaani alimueleza Rais Kikwete kwamba moja ya vitu vilivyomkwamisha kuwaletea maendeleo makubwa wananchi ni watendaji wabababishaji waliokuwemo kwenye ofisi nyingi wakati wa utawala wake na akaahidi kukabiliana vilivyo na changamoto hiyo.
Katika kufikia lengo hilo, alisema ingawa kwa wakati wote yeye na mgombea mwenza walikuwa wakiinadi ilani ya CCM, katika kuliletea Taifa maendeleo kila mtu anapaswa kutekeleza wajibu wake kwa uaminifu.
Ili kusisitiza juu ya azma yake ya kusimamia utendaji serikalini, Dk Magufuli alisema siku atakapoapishwa, ataanza kazi mara moja kwani tayari ameshatembezwa sehemu zote za Ikulu na Rais anayemkabidhi kijiti cha uongozi, na hivyo kilichobaki ni utekelezaji wa mipango yake kwa vitendo.
“Nimeona nilisema hili mapema ili lisiniletee kiungulia.”
Dk Magufuli, ambaye amewahi kuwa Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo pamoja na Wizara ya Ujenzi, alikumbusha changamoto nyingi alizokutana nazo sehemu alizopita na kubainisha kuwa jukumu zito alilokutana nalo ni kuwasafisha watendaji ambao hawawajibika ipasavyo.
Alisema kazi hiyo ilimuweka kwenye wakati mgumu na kuahidi halitajirudia akiwa madarakani.
Aliwashukuru Watanzania kwa uaminifu waliouonyesha kwake na mgombea mwenza, Samia Hassan Suluhu kwa kuwapa ridhaa ya uongozi kwa miaka mitano ijayo na kueleza kwamba ushindi huo si wa CCM pekee bali wananchi wote kwa jumla.
Alisema hiyo inatokana na ukweli kwamba licha ya kwamba kwenye baadhi ya maeneo wapinzani walishinda nafasi za udiwani na ubunge, kwenye urais walimpa yeye ili awe na wajibu wa kuwatumikia kwenye nafasi hiyo ya juu zaidi katika uongozi wa nchi.
Pamoja na changamoto zote zilizojitokeza wakati wa mchakato wa uteuzi mpaka kampeni, Dk Magufuli alisema kuna wajibu wa kuijenga upya CCM kwani kuna mambo yanakwenda ndivyo sivyo na yasipofanyiwa kazi mapema yatakiangusha chama hicho.
“Kwenye kampeni za mwaka huu tumepata changamoto nyingi sana na baadhi zilitoka ndani ya wana-CCM. Hakuna haja ya kuwa na idadi kubwa ya wanachama wakati kuna wanafiki,” alisema Dk Magufuli, ambaye kwa mujibu wa utaratibu wa chama hicho, Rais hutakiwa kuwa mwenyekiti.
“Samahani Rais wangu. Ukiona mnafiki, mfukuze mara moja. Ni rahisi kupambana na adui aliye nje kuliko wa ndani. Hakuna haja ya kuwa na wanachama wengi wanafiki, ni bora wabaki wachache lakini waaminifu.
“Nisiposema nitakuwa mnafiki, msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Watubu wajirekebishe. Ni heri mara kumi kuwa na mpinzani kutoka nje kuliko ndani ya chama. Mipango yenu mtaipanga mchana usiku wataitoa nje, ni afadhali uwe na mchawi atakuroga ufe kuliko mnafiki ndani.”
Dk Magufuli aliwahi kutoa kauli kama hiyo wakati wa kampeni zake aliposema kuwa baadhi ya wanachama walikuwa naye mchana, lakini usiku walikuwa Ukawa.
Huku akishangiliwa, Dk Magufuli alimgeukia Kikwete na kusema: “Wewe ni mwenyekiti, lakini ulikaa na wanafiki ndani ya CCM. Hao ndiyo wametufanya wakati mwingine tufike hapa tulipofika.”
Hata hivyo, Dk Magufuli aliwataka wale wote walioasi warejee kwenye chama ili kwa pamoja, waweke mikakati itakayokiimarisha chama kinachoongoza dola wakati kikiwatumikia wananchi waliokiamini kwa moyo mkunjufu.
Pamoja na watu wengine, aliwashukuru wasanii waliozunguka naye mikoani wakati wa kampeni za kujinadi kwa mchango wao mkubwa ambao alisema ulifanikisha ushindi unaompeleka Ikulu.
Kuanza kazi haraka
Dk Magufuli aliwahakikishia wananchi kuwa mara baada ya kuapishwa, ataanza kazi kwa kuwa hakuomba nafasi hiyo kwa majaribio bali kuwatumikia wananchi kwa dhati.
Pia ameomba ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi ili waweze kufanikisha utekelezaji wa ilani kwa yale ambayo ameahidi wakati wa kampeni yeye na Makamu Rais Samia Suluhu Hassan, ili waweze kutimiza wajibu wa kuwatumikia bila kinyongo na kuyatimiza yake waliyoahidi wakati wa kampeni.
“Kwa hiyo niwaombe ndugu zangu Watanzania wote bila kujali vyama vyetu, tunaomba sana ushirikiano wenu , tusipopata ushirikiano wetu hatuwezi kuyatimiza kwa wakati. Tusipopata ushirikiano mzuri kutoka kwenu, mtatuchelewesha,” alisema.
Alisema kero walizoziona kwa wananchi ni maji, umeme, miundombinu, ambazo alisema wananchi wanataka zitatuliwe haraka.
Amsifu JK
Dk Magufuli alimsifu Rais Jakaya Kikwete akisema: “Nataka niseme mheshimiwa Rais una moyo wa pekee, Mungu akujalie sana. Viongozi wengi Afrika wanapokaribia kuondoka madarakani wengine huwa wanatengeneza hata katiba tofauti ili waendelee kubaki madarakani, lakini wewe upo tayari kuondoka hata leo.”
Dk Magufuli alisema anaamini kwamba wananchi wataendelea kumuombea kwa kuwa amethamini Tanzania kwanza, hivyo ataendelea kuhitaji busara zake pale itakapobidi.
Rais Kikwete
Awali, Rais Kikwete alitupa kijembe kwa baadhi ya makada wa CCM waliokihama chama hicho baada ya kutemwa kwenye kura za maoni, akisema hawakuweza kutimiza ndoto zao.
Kikwete alisema nafasi hiyo haipatikani kimasihara na kwamba juhudi kubwa hufanywa kabla ya kupatikana kwa mteule ambaye atatumikia wananchi bila kujali itikadi zao, dini wala kabila.
“Tumempata Rais mteule. Sasa tushirikiane kuijenga nchi yetu. Kulikuwa na wengi waliojitokeza hata wengine wakathubutu kuhama chama wakiamini wameonewa, lakini hata walikokwenda wameukosa urais,” alisema Kikwete.
“Tumempata mbadala wangu, mlisema mimi mpole sasa huyu ni tingatinga.”
UN yampongeza
Katika hatua nyingine, salamu za pongezi zimeanza kumiminika baada ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon kuipongeza Tanzania kwa kufanya uchaguzi wake kwa amani na kusema huo ni mfano kwa nchi zinzotekeleza demokrasia ya kweli.
Katika taarifa yake iliyotumwa kwa vyombo vya habari, Ki-moon ameeleza kufurahishwa kwake na utulivu ulioonyeshwa na Watanzania wakati wote, kuanzia upigaji kura, kuzihesabu mpaka utangazaji wa matokeo.
“Uvumilivu mliouonyesha umethibitisha uzingatiaji wenu wa demokrasia, amani na utulivu. Kilichotokea Zanzibar kinavuta macho yangu pia, napenda kushauri njia za maridhiano ya kupata muafaka kwa changamoto yoyote inayojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu,” inasema taarifa hiyo. SOMA ZAIDI KUPITIA Gazeti la  MWANANCHI

DK. JOHN POMBE MAGUFULI AKABIDHIWA CHETI CHA USHINDI WA URAIS WA TANZANIA AWAMU YA TANO JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia), akimkabidhi cheti cha Urais Rais Mteule wa Tanzania Dk.John Magufuli katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam leo. Kushoto ni Makamu wa Rais Mteule, Samia Hassan Suluhu.
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia), akimkabidhi cheti cha Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu katika hafla hiyo.
 Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli (kulia), akiwapungia mkono wananchi wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa cheti cha urais. Kutoka  kushoto ni mgombea urais kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira na mgombea nafasi hiyo kupitia Chama cha ADC, Chief Lutalosa Yemba.
 Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi (kushoto), akimpongeza Rais Mteule wa Tanzania Dk. John Magufuli baada ya kuchaguliwa kuwa rais.
 Makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakishangilia wakati Rais Mteule wa Tanzania Dk.John Magufuli alipokuwa akitoka Ukumbi wa Diamond Jubilee kukabidhiwa cheti cha urais.
 Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo.
  Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Magufuli akimuonesha Rais Jakaya Kikwete cheti cha ushindi.
 Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Makufuli akiwa katika picha ya pamoja na wagombea urais wenzake wa vyama vingine.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva kwa kusimamia vizuri uchaguzi mkuu wa 2015.
Rais Jakaya Kikwete na Rais Mteule Dk.John Pombe Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na wake zao kwenye hafla hiyo.

Na Dotto Mwaibale

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemkabidhi cheti cha ushindi aliyekuwa mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk, John Magufuli baada ya kushinda kwa kura nyingi kuliko wenzake kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Aidha wanasiasa wamemtaka Dk. Magufuli kutekeleza mambo yote ambayo ameahidi, huku Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo Anna Mghwira., akimtaka ahakikishe kuwa Katiba ya wananchi inapatikana ili kufanikisha dhana ya mabadiliko ambayo yalikuwa yanatajwa na wagombea wote.

Akizungumza kabla ya kumkabidhi cheti hicho katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam leo Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki huku akiwapongeza wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura tofauti na mwaka 2010.

Lubuva alisema katika uchaguzi huo wagombea wa nafasi ya urais ni Anna Mghwira wa ACT, Chief Lutalosa Yemba wa ADC, Dk. Magufuli wa CCM, Edward Lowassa wa Chadema, Hashim Rugwe wa Chaumma, Malik Kasambala wa NRA, Elifatio Lyimo wa TLP na Fahmi Dovutwa wa UPDP.

Alisema, tume imemtanga Dk. Magufuli kwani amefanikiwa kupata kura nyingi kuliko wagombea wenzake ambapo  walioandikishwa ni wapigakura 23,161,440, waliopiga kura ni 15,589,639 sawa na asilimia 67,31 ya waliojiandikisha.

Alisema kura halali ni 15,193,862 sawa na asilimia 97.46, kura zilizokataliwa ni 402,248 sawa na asilimia 2.58.

Jaji Lubuva alitangaza matokeo kuwa Mghwira amepata kura 98,763 sawa na asilimia 0.65, ADC amepata kura 66,049 sawa na asilimia 0.43.

Dk. Magufuli amepata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46 sawa na asilimia 58.46, Lowassa amepata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97, Rungwe 49,256 sawa na asilimia 0.32, Kasambala amepata kura 8,028 sawa na asilimia 0.05.

Wengine ni Lyimo amepata kura 8,198 sawa na asilimia 0.05, Dovutwa amepata kura 7,785 sawa na asilimia 0.05.

Kailima

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Ramadhan, alisema kura zilizopigwa zinatoka katika majimbo ya uchaguzi 264 na kata 3,957 na hakuna dosari kubwa ambayo ilitokea.

Alisema katika nafasi ya ubunge majimbo yaliyofanya uchaguzi ni 256 huku majimbo nane yakiwa hayajafanya uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali ambazo ni vifo kwa wagombea na karatasi za wagombea kuwa na mapungufu.

Kailima alisema pia kuna Kata ambazo hazijafanya uchaguzi kutokana na mapungufu mbalimbali ambapo wanatarajiwa kufanya uchaguzi mapema iwezekanovyo.

"Mchakato  wa uchaguzi umefanyika kwa kufuata sheria hivyo tume inadiriki kusema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki kwani hakuna lalamiko lolote kutoka kwa wakala," alisema.

Alisema kifungu cha 85 kinaipa mamlaka haki ya kutangaza matokeo hata kama baadhi ya wagombea watagoma kusaini matokeo husika hivyo aliyetangazwa na tume ndiye mshindi.

Mghwira

Akizungumza baada ya tume kumkabidhi mshindi cheti, aliyekuwa mgombea wa urais kupitia ACT-Wazalendo, Anna Mghwira, alisema anakubaliana na matokeo na kumtaka Magufuli ahakikishe kuwa anasimamia upatikanaji wa katiba.

Mghwira alisema, iwapo anataka mabadiliko yaweze kupatikana ni jukumu lake kusimamia upatikanaji wa katiba ya wananchi kwani ndiyo inaweza kuleta mabadiliko sahihi kwa Tanzania ya leo.

Aidha, alimtaka mshindi huyo wa nafasi ya urais kusimamia suala la usawa na umoja wa kitaifa ambao utaweza kujenga nchi kufikia maendeleo sahihi pamoja na wananchi.

"Tunahitaji uchumi imara ili kurejesha fahari ya nchi na wananchi kwani hakuna shaka kuwa wananchi wamekata tamaa na taifa lao jambo ambalo sio sahihi," alisema.

Mghwira alitumia nafasi hiyo kumkabidhi Dk. Magufuli, ilani ya chama hicho kwani ina malengo ya kuibadilisha Tanzania.

Yemba

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea urais, kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Chifu Litalosa Yemba, alisema anampongeza Dk. Magufuli kwa ushindi huku akiweka bayana kuwa tangu aanze kushiriki chaguzi uchaguzi wa mwaka huu ndio uchaguzi ambao ulikuwa huru na wa haki.

Alisema mapungufu ambayo yanalalamikiwa na baadhi ya wagombea yanapazwa kuangaliwa kwa undani zaidi ili kuhakikisha kuwa hayarejei kutokana na ukweli kuwa mchakato huo ni muhimu kwa wananchi.

Yemba alisema, anampongeza mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, kwa kufanya kampeni za kistaarabu pamoja na matusi, kashfa na dharau ambazo zimejitokeza kwake.

"Tunaweza kusema mambo mengi ila ambaye ahataki kutambua mchango wa Lowassa katika siasa za Tanzania hasa upinzani atakuwa hajui siasa ninachoomba Chadema na vyama vya upinzani kudumisha nguvu hii kwani hatujaweza kupata kura zaidi ya milioni 2 tangu kuanza kwa vyama vyetu," alisema.

Aidha, ameweka bayana kuwa iwapo angefanya kampeni katika uchaguzi huu angeweza kuwa mshindi wa pili lakini kutokana na uhaba wa fedha walishindwa kufanya kampeni ila anawashukuru wananchi kwa kura ambazo wamepata.

Jonatha

Akizungumzia uchaguzi huo Kiongozi wa waangalizi kutoka Jumuia ya Madola, Rais mstaafu wa Nigeria, Godluck Jonathan, alisema uchaguzi ulikuwa huru na haki na kuzitaka nchi zingine kuiga Tanzania kwani imekuwa mfano bora.

Godluck alisema, uchaguzi ni jambo ambalo linakuwa na changamoto mbalimbali ambapo sio jambo rahisi kila mtu kukubaliana na matokeo lakini kwa mtazamo wao wanaamini kuwa uchaguzi huo umefanyika vizuri.

Nchemba

Mwigulu Nchemba ambaye ni mbunge mteule wa Jimbo la Iramba Magharibi, alisema amefurahishwa na ushindi huo kwani Dk. Magufuli ana vigezo vyote vinavyohitajika kwa kiongozi wa nchi.

Alisema watanzania wajiandae kwa kupata mabadiliko sahihi ambayo walikuwa wanayataka kwani kiongozi huyo ni mtu ambaye anasimamia uwajibikaji, uadilifu na mchapakazi.

"Vigezo vimetumika kumpata rais sahihi kwa maslahi ya Taifa, hivyo kilichobakia ni watu kufanya kazi ili dhana nzima ta hapa kazi tu ionekane na mabadiliko pia," alisema.

Mwijage

"Huyu ndiye chaguo sahihi kwa maslahi ya Taifa na pia naamini hata Mungu ndiye aliyetaka tumpate Magufuli naamini mabadilikio yataanza vijijini ili kuzuia watu kuja mijini kutafuta kazi," alisema.

Alisema watu wajiandae kufanya kazi kwani kasi ya kiongozi huyo mpya wa nchi itakuwa haina mzaha hivyo wale wakaa vijiweni watambue kuwa nafasi hiyo haipo kupitia Dk. Magufuli.

Madabida

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, alisema ushindi huo wameupokea kwa furaha pamoja na ukweli kuwa yalikuwa ndio matarajio yao.

"Sisi hatukuwa na shaka kuhusu ushindi huo lakini pia mgombea wetu ni mtu mzuri sana katika utendaji naamini kuwa wananchi wamemuelewa hivyo watarajie kuona mabadiliko ya kweli," alisema.

Madabida alisema vyama vya upinzani vilikuwa vinatumia nguvu ya hali ya juu kuhakikisha kuwa vinashinda lakini kutokana na mikakati yao wamefanikiwa kuibuka kidedea.

Kuhusu majimbo mengi ya mkoa wake kuchukuliwa na vyama vya upinzani alisema hayo ni maamuzi ya wananchi lakini wao kama uongozi walifanya kila linalowezekana kufanikisha ushindi.

Aidha, alikanusha taarifa za kuwa wameshindwa kutokana na yeye kumuunga mkono Lowassa wakati yupo CCM na kuwa hakufanya kampeni na kuweka bayana kuwa alikuwa anamuunga mkono wakati huo ila kwa sasa alikuwa na Magufuli.

Katika hafla hiyo ya kumkabidhi cheti cha ushindi Dk. Magufuli na Makamu wake Samia Suluhu Hassan, pia Rais Jakaya Kikwete, alishiriki, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Spika wa Bunge Anne Makinda, Rais wa Awamu ya Pili, Ally Hassan Mwinyi, Mawaziri Wakuu wastaafu na viongozi wengine walihudhuria pamoja na wananchi na wanachama wa CCM.

Friday, October 16, 2015

BOHARI YA DAWA (MSD) YASHIRIKI KONGAMANO LA 29 LA WANASAYANSI WATAFITI MAGONJWA YA BINADAMU


  Ofisa Uhusiano wa MSD, Benjamin Massangya akimuonesha Mwananchi aliyetembelea banda la MSD  nembo ya MSD iliyowekwa katika makasha na vifungashiyo vya dawa.
 Mtaalamu wa Maabara kutoka Bohari ya Dawa (MSD), Twahiri Magoolo  (kushoto), akimuelekeza jambo mwananchi  aliyetembelea banda la MSD katika kongamano la 29 la wanasayansi wa utafiti wa magonjwa ya binadamu Dar es Salaam jana. Kongamano hilo liliandaliwa na Taasisi ya Utafiti  Magonjwa ya Binadamu (NIMR).
Dawa na vifaa mbalimbali vikiwa katika banda la MSD katika kongamano hilo.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

SERA ZA WAGOMBEA ZINAPOGUSA SUALA LA KUPUNGUZA AJALI BARABARANI.

Tambua ni kwa kiasi gani sera za wagombea kutoka vyama mbalimbali zimegusia saula la kupunguza ajari za barabarani: Serikali Yasaini Mkataba Wa Ujenzi Wa Barabara Za Juu.

DK. MAGUFULI APOKELEWA KWA NDEREMO NA VIFIJO KISARAWE NA UKONGA WAKATI WA MKUTANO WA KUOMBA KURA

 Wananchi wa Jimbo la Kisarawe, mkoani Pwani wakishangilia hotuba ya Dk Magufuli  wakati wa mkutano wa kampeni mjini Kisarawe leo. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Kisarawe, Seleman Javo wakati wa mkutano wa kampeni mjini Kisarawe leo.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Kisarawe.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akionyesha picha aliyochorwa.mm
 Wakazi wa Mombasa, Ukonga, Dar es Salaam wakiuzuia msafara wa Dk Magufuli ulipokuwa ukitoka Kisarawe kwenda eneo Moshi Bar kuendelea na kampeni.
 Shamra shamra za kumpokea Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli mapema leo, wakati akielekea Ukonga katika barabara ya Moshi - Bar.
 Msafara wa Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli ukipokelewa kwa nderemo na vifijo.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiingia Ukonga katika mkutano wake wa kuomba kura.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Ramadhan Madabida  akimnadi Dk. Magufuli kwa wakazi wa Ukonga.
 Akina mama wakiwa na nyuso za furaha.
 Umati wa watu waliohudhuria mkutano huo.
Kila mmoja akitaka kumuona mgombea.
Dk. Magufuli akitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Mombasa hadi Moshi Baa kwa kiwango cha Lami.
 Mmoja ya wafuasi wa CCM akisiliza sera za mgombea Urais wa Tanzania, Dk. John Magufuli huku akiwa amebeba mboga mboga zake.
  Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akinyooshewa vidole gumba na wakazi wa Jimbo la Ukonga ikiwa ni ishara ya kukubali kumpigia kura ya ndiyo , wakati wa mkutano wa kampeni eneo la Moshi Bar, Ukonga Dar es Salaam.
Dk. Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Ukonga kupitia CCM, Jerry Silaa wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo. Dk. Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Jimbo la Ukonga kupitia CCM wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo.