Monday, September 27, 2010

Frank Lampard kukosa mechi muhimu

Frank Lampard atakosa michezo muhimu kwa timu yake ya Chelsea na timu ya taifa ya England kutokana na kuendelea kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa ngiri.

Lampard mwenye umri wa miaka 32 hajaichezea klabu yake kwa mwezi mmoja na meneja wake Carlo Ancelotti amethibitisha kiungo huyo hataweza kucheza kwa takriban wiki mbili zijazo.

Kipindi hicho atakosa mechi dhidi ya Marseille, Arsenal na mchezo wa kufuzu mashindano ya Euro 2012 wakati England itakapopambana na Montenegro.

Ancelotti ameendelea kusema, Lampard hawezi kucheza kwa sasa, wanahitaji muda zaidi tofauti na walivyotazamia.

Kwa vile hajaichezea Chelesea, Ancelotti amesema vile vile hatakuwa tayari kuichezea timu ya taifa.

Lampard alirejea mazoezini baada ya kufanyiwa upasuaji tarehe 31 mwezi wa Agosti, lakini amekuwa akisumbuliwa na maumivu kwenye kovu.

Tayari amekosa mechi za England walizoshinda za kufuzu michezo ya Euro 2012 dhidi ya Bulgaria na Switzerland mapema mwezi wa Septemba na pia atakosa mechi dhidi ya Montenegro katika uwanja wa Wembley tarehe 12 mwezi wa Oktoba.

Mara ya mwisho kuichezea Chelsea ilikuwa tarehe 28 mwezi wa Agosti timu hiyo ilipoifunga Stoke mabao 2-0.

Papa wa Misri awaomba radhi Waislamu

Kiongozi wa kikiristo wa madhehebu ya Copti nchini Misri ameomba radhi kwa matamshi "yasiofaa" yaliyotolewa na askofu aliyoonesha kuwa na wasiwasi na baadhi ya aya za Quran.

Papa Shenouda III alisema kupitia televisheni ya taifa, " Ninaomba samahani sana kuwa hisia za ndugu zangu wa kiislamu zimeumizwa."

Awali, askofu Bishoy alisema- tofauti na imani za Muislamu- baadhi ya aya za Quran huenda ziliongezwa baada ya kifo cha Mtume Muhammed.

Mamlaka ya kiislamu ya al-Azhar nchini humo yamesema matamshi hayo yanatishia usalama wa kitaifa.

Imam Ahmed al-Tayyeb katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumamosi na al-Azhar, moja ya kituo muhimu ya mafunzo ya kidini ya madhehebu ya Sunni, " Tabia ya namna hii haifai na inatishia usalama wa taifa katika wakati ambao ni muhimu kuulinda."

Alikuwa akijibu baada ya taarifa kutolewa na vyombo vya habari vya Misri ambapo askofu Bishoy, ambaye ni wa pili kwa nafasi za upadri katika kanisa hilo la Copti, alipohoji aya za Quran kupinga Umungu wa Yesu Kristo.

Askofu huyo aliripotiwa akisema aya hizo ziliwekwa na mmoja wa maswahaba zake Mtume Muhammed baada ya kifo chake.

Waislamu wanaamini kuwa aya zote za Quran zilidhihirishwa kwa mtume kupitia malaika Jibril na ni neno la Mungu lisiobadilika.

Papa Shenouda alisema katika mahojiano ya televisheni siku ya Jumapili, " Midahalo ya imani za kidini ni mwiko, mwiko kabisa."

Aliongeza, "Suala la kuibua mijadala hiyo si sawa, na kulizungumzia zaidi haifai."

Ijapokuwa Waislamu na Wacopt wa Misri aghlabu huishi kwa amani, wasiwasi unazuka juu ya kujengwa makanisa mapya na matukio ya kubadili dini.

Idadi ya wafuasi wa madhehebu ya Copt ni kuanzia asilimia sita hadi 10 ya raia milioni 80 nchini humo na hulalamika juu ya ubaguzi unaofanywa na taifa hilo.

Thursday, September 23, 2010


Mlinzi wa Sunderland Titus Bramble, amekamatwa baada ya mwanamke kubakwa kwenye hoteli moja mjini Newcastle.

Mchezaji huyo wa Ligi Kuu ya England amekamatwa pamoja na mtu mwengine katika hoteli ya Vermont mapema siku ya Jumatano na wanahojiwa na polisi.

Bramble mwenye umri wa miaka 29 amekamatwa kwa kushukiwa amebaka baada ya polisi kupigiwa simu na mwanamke mmoja.

Klabu ya Sunderland hadi sasa haijazungumza lolote kuhusiana na tuhuma hizo. Bramble alijiunga na klabu hiyo akitokea Wigan msimu huu.

Msemaji wa kituo cha polisi cha Northumbria, amesema wanaume wawili, wakiwa na umri wa miaka 29 na 30 wamekamatwa wakituhumiwa kubaka mwanamke.

Bramble pia aliwahi kuichezea New Castle na Ipswich.

JE ARSENAL WANAONEA WANYONGE?

Katika mechi tatu Arsenal wamefikisha jumla ya magoli 16. Walipocheza dhidi ya Braga ya Ureno walitikisa magoli mara sita, kabla ya hapo waliichapa Bolton Wonderers goli 4-1, awali Blackpool walipigwa 6-0.

Arsene Wenger anaamini timu yake imejengeka zaidi na itapata mafanikio, lakini amesikika akisema hivyo miaka kadhaa bila kuambulia kitu.

Maswali ambayo yanaibuka ni je Arsenal inaonea wanyonge? Wakipambana na timu kali kama Chelsea, Man U au Real Madrid na Barcelona watafurukuta kwa kasi hiyo waliyo nayo sasa?

Ni wazi kuwa safu ya ulinzi msimu huu imeimarika zaidi kuliko wakati Mikael Sylvestre na Sol Campbell na William Gallas walipokuwa wakicheza katikati. Lakini kama ni Arsenal kuonea wanyonge, iweje pasipo Robin van Parsie, Theo Walcott, Thomas Vermaelen, Abu Diaby na wengineo, bado wanaweza kufunga magoli sita katika mechi moja?

Huenda ni mapema sana kuhoji uimara wa Arsenal. Lakini meneja Arsene Wenger anasema ana imani kikosi chake kimejengeka na kipo tayari kukwaruzana na timu yoyote kubwa au ndogo.

Kwa jinsi walivyocheza mechi ya ligi ya vilabu bingwa barani Ulaya dhidi ya Braga, Arsenal wanacheza soka ya kuvutia, lakini mara nyingi soka hiyo imegeuka kuwa maumivu wanapocheza na timu zisizokuwa na masihara mbele ya goli.

Na je Arsene Wenger amesikika mara ngapi akisema "chipukizi wake" watabeba kikombe au vikombe? Tunachoweza kufanya kwa sasa, ni kusubiri mwisho wa msimu.

Friday, September 10, 2010

MWISHO KATIKA HATIHATI..BBA

In her Diary Session, Meryl reveals how she considered saving Mwisho but reminded herself she walked into the house as an individual.
Meryl, who is Head of House this week, mentioned how she feels there is no room for personal issues when it comes to playing the game. Meryl, who was also up for possible Eviction, switched herself and put Paloma up instead.
She mentioned how if Mwisho has to leave, they will leave as friends and family and will see each other outside the house. "We are here to play the game are we not," she said.

Meryl also took the time out to send a shout out to her daughter who turned 10 months on Sunday and also addressed how she feels Kaone has not been following the rules of his punishment to the tee.

BAADA YA MIAKA 9 YA UJANE UPENDO NKONE KUOLEWA TENA MWEZI UJAO.

Muimbaji wa nyimbo za Injili(Gospel) Upendo Nkone (pichani) anatarajiwa kufunga ndoa tarehe 17 October 2010 na Mchungaji John Mbeyela ambaye pia ni mjane mwenye watoto watatu.Ndoa hiyo itafungwa katika kanisa la Naioth kwa Mchungaji Mwasota.

Kwa mujibu wa mtandao wa Strictly Gospel,ndoa hiyo inakuja baada ya miaka 9 ya kuwa mjane. Upendo Nkone tayari anazo albamu tatu kibindoni zikiwa ni Mungu Baba,Hapa Nilipo na Zipo Faida.

We wish them all the best.

Photo Courtesy of Waimbaji wa Muziki wa Injili Tanzania Photostream

Monday, September 6, 2010

KASHFA YA KUPANGA MATOKEO YA KRIKETI UINGEREZA.

Gazeti moja la Uingereza limetoa madai mapya kuhusu kashfa ya kupanga matokeo ya mechi inayomhusisha mchezaji cricketi wa Pakistan.

Gazet hilo, The News of the World linadai Baraza la Kimataifa la Cricket -lCC-linamchunguza mchezaji huyo, ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu za kisheria.
Baraza la ICC limesema haliwezi kutoa taarifa yoyote juu ya uchunguzi unaondelea.

Hatua ya kupanga matokeo ya mechi ni nzito kuliko madai yaliyotolewa na gazeti hilo wiki iliyopita.

Gazeti hilo lilifichua kashfa ya kamari ambayo ilisababisha wachezaji watatu wa timu ya Pakistan kusimamishwa na wanafanyiwa uchunguzi na Baraza la Kimataifa la Cricketi pamoja na polisi.

Friday, September 3, 2010

MAJIBU YA KIKAO CHA SIMBA KILICHOFANYIKA MWANZA JUMATANO WIKI HII

WANACHAMA WA SIMBA SPORT CLUB TAWI LA MWANZA WAMEJIPANGA KIKAMILIFU KATIKA KUIPOKEA TIMU YAO, KUIPA HIFADHI YENYE HADHI CLUB HIYO YA SOKA INAYOSHIRIKI LIGI KUU ILI IPATE USHINDI WA KISHINDO KWA MECHI ZAKE NNE ITAKAYOCHEZA WAKATI IKITUMIA UWANJA WA CCM KIRUMBA MWANZA KAMA UWANJA WA NYUMBANI.

AKIZUNGUMZA NA CLOUDS FM MAKAMU MWENYEKITI WA SIMBA TAWI LA MWANZA AMBAYE ANATOKA KATIKA KUNDI LA FRIENDS OF SIMBA AMESEMA KUWA UONGOZI WAKE PAMOJA NA WANACHAMA WA MWANZA NA UKEREWE WAMEJIPANGA KIKAMILIFU KUHAKIKISHA KUWA TIMU YAO INASHINDA NA KUCHUKUWA POINTI ZOTE PINDI ITAKAPO TIA TIMU JIJINI MWANZA.

ISHU ALIONGEZA KWA KUSEMA KUWA MWAKA JANA WANACHAMA WA SIMBA TAWI LA MWANZA WALIHAKIKISHA KUWA SIMBA INAENDELEZA WIMBI LAKE LA USHINDI NA KUTOFUNGWA MECHI HATA MOJA KWA KUHAKIKISHA WANAJIPANGA VYEMA NA KUKAMILIKA KILA IDARA, BASI VILE VILE MWAKA HUU NDIVYO ITAKAVYO KUWA.

KUHUSU USHINDANI WA JADI ULIOPO WA TIMU YAKE NA WANA KISHAMAPANDA (TOTO AFRIKA), ISHU ASHRAF AMEIPONDA TIMU YA TOTO KWA KUSEMA KUWA LICHA YA MABADILIKO YA USAJIRI KWA TIMU HIYO KUCHUKUWA WACHEZAJI WENYE VIPAJI, TIMU HIYO SI CHOCHOTE, SI LOLOTE KWA MNYAMA NAKUAHIDI KUWAFUNDISHA SOKA TOTO PINDI WATAKAPO KUTANA ANA KWA ANA DIMBANI.

TIMU YA SIMBA INAYOTEGEMEA KUWASILI MWANZA ASUBUHI YA TAREHE 12 SEPT 2010 KWA USAFIRI WA ANGA, IMEUTEUWA UWANJA WA CCM KIRUMBA WA JIJINI MWANZA KUWA UWANJA WAKE WA NYUMBANI KUPISHA UKARABATI KATIKA UWANJA WA BIBI DAR ES SALAAM.

Wednesday, September 1, 2010

ASAMOAH GYAN HUYOO SUNDERLAND.

Ghana striker Asamoah Gyan completed his move to English Premier League club Sunderland for a club record fee of over 13 million pounds on Tuesday.

Gyan agreed a four-year contract with Steve Bruce's side in a deal which shatters the club's previous record when they signed Darren Bent from Tottenham for 10 million pounds in 2009.

The 24-year-old's move was announced 20 minutes before the transfer window in England shut at 1700GMT.

"Sunderland have broken their transfer record to sign Ghanaian World Cup star Asamoah Gyan from French Ligue 1 side Stade Rennes," a statement on the club's website confirmed.

"Gyan arrives on Wearside for a fee in excess of 13 million pounds - more than Sunderland chief Steve Bruce paid to acquire Darren Bent from Tottenham last year."

Gyan boosted his reputation with some fine displays at the World Cup scoring three goals, although his tournament ended on a low note when he missed a last-minute penalty against Uruguay that would have sent Ghana into the semi-finals.

The Accra-born star has netted 22 times in 44 international appearances and his move to the Premier League should be eased by the presence at Sunderland of Ghana team-mate John Mensah, who is loan from French club Lyon.

Gyan could make his Sunderland debut at Wigan on September 11 in the team's next game after the international break.

He is already looking forward to playing in the local derby against Newcastle and told the club's website: "It's been a long day, but finally I'm happy to be here.

"My family is in England already and I am happy this is the right place for me.

"The Sunderland coach has faith in me because he has been following me for two years now. I am pleased I have the opportunity to come to England.

"I follow English football and I know Sunderland have incredible fans.

"I especially know about the derby when they play against Newcastle. That is something incredible. I have witnessed that myself."

Gyan's arrival was perfectly timed as Bruce learned on Tuesday that striker Fraizer Campbell will be sidelined for at least six months after rupturing cruciate knee ligaments.