Monday, December 26, 2011

MANENO OSWARD VS RASHIDI MATUMLA AKUNA MBABE POINT 99 KWA 99 DROO

Bondia Rashidi Matumla (kushoto) akiwa chini baada ya kuteleza uku mpinzani wake Maneno Osward akimsubili kwa ajili ya kumpiga wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano point ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo.

Bondia Rashidi Matumla (kushoto) akiwa chini baada ya kuteleza uku mpinzani wake Maneno Osward akimsubili kwa ajili ya kumpiga wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano point ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo.

Bondia Rashidi Matumla (kushoto) na Maneno Osward wakioneshana ufundi wa kutupa masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano point ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo.

Bondia Maneno Osward (kushoto) akimuacha Rashidi Matumla chini baada ya kuanguka kwa kuteleza wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana wakati wa sikukuu ya Xmasi mpaka mwisho wa pambano point ni 99 kwa 99 hivyo kuwa droo.(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)

Saturday, December 24, 2011

AMINI USIAMINI KITU KIPYA CHENYE HADHI YA KITALII NA BEI NAFUU NDANI YA MAGU MWANZA

Ni kiota kipya kabisa kimefunguliwa ndani ya wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza eneo linaitwa Cadillac hotel.

Mazingira mazuri ndani na nje huku ukipatiwa huduma safi toka kwa wahudumu waliobobea.

Korido za kuelekea vyumbani.

Cadillac mazingira.

Flamingo ni Moja ya vyumba classic hotelini hapa.

Usingizi mwananaZZZzzzz!!!

Suitabo bediZZZzz!!

Ukumbi wa kisasa wa mikutano unapatikana hapa.

Bustani bar iliyosheheni mashamsham ya pekee.

Hii ni bar yenye kila aina ya vinywaji inayopatikana ndani ya bustani tuliiivu Cadillac Magu Mwanza.

Kwa mawasiliano zaidi piga
simu +255282530300
mobile +255786777618

Tuesday, December 13, 2011

HAPPY BIRHTDAY FATMA SHEMWETA WA STAR TV

Huu ndiyo Mkate wa nakshi ya sukari wa Fatma Shemweta katika sherehe ya siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika ukumbi wa VIP The New Stone Club Mwanza.

Fatma na Husna.

Mtangazaji wa Star Tv Fatma Shemweta (R) na shosti wake The Platnum (L).

ZE MilipukozZZZz!!

ChiazZZZzzz!!!

Kitu cha Dance' pale kati.

Kutoshea idadi keki ilikatwa 'mapande makumi mawili na saba'.

Fatma akilishwa keki na Beste'.


To the Mc.

Tamu ya mkate wa sukari.

www.gsengo.blogspot.com

Meneja wa The New Stone Club, Dj Ally Coco naye alionja utamu wa keki.

Keki kwa dada.

The Big Top Ten akilishwa keki.

Platinum na shukurani kwa mtoto.

Mtoto akipokea zawadi spesheli.

Mtu muhimu sana' Mr Kaiza naye alijumuika vyema tena sana.

Mc wa shughuli alikuwa na mikogo kinomanoma, na hili ndilo pozi la kukabidhi mzigo.

The Crew na Sahara Communication.

Safu ya mashosti...

Friday, December 2, 2011

MIAKA 12 YA KUZALIWA KWA CLOUDS FM RADIO YA WATU KIBAO...................................!

Bwiga wa Mbwiga na Timu ya Sports X-Tra akipata kipande cha keki huku akishuhudiwa na na Ephraim Kibonde, Edo Kumwembe na Shaffi Dauda.

Kutoka kushoto Kibonde, Edo Kumwembe, Shaffi Dauda, Mbwiga, Alex luambano, Joff Lea na Abdul Mohamed.

Kipindi cha XXL nacho kilijitanua mida yake kutoka shoto ni B.12, Bobb Jurnior, Madee na Dj Fetty.

Adam Mchomvu aka 'Baba JONIii' (R) akijitanua na Maunda Zoro (kati) naye Mwalimu wa Waalimu Banza Stone.

THE CREW wakipata flash.

Leo Tena si ndiyo hawa Gea Habib(L), Dina Marious(C) na Husna Abdul(R).

"Amka kumekuchaaaa" PJ(L), Babra Hassan(C) na Bonge(R).

Shughuli ilianzia asubuhi katika kipindi cha Power breakfast na Hapa PB ilikuwa ikiisha na wakatukaribisha timu leo tena.

Monday, November 28, 2011

TWANGA PEPETA YADONDOSHA MAKOMBORA KUAMSHA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU LONDON

African Stars Entertainment Tanzania(Aset) ambao wanajulikana kwa jina la “Twanga Pepeta” walikuwa kivutio cha sherehe za miaka 50 ya Uhuru London juzi Jumamosi. Kikosi hiki cha watumbuizaji maarufu wa Kibongo kilikaribishwa na Urban Pulse, Jestina George wakishirikiana na Ubalozi wa Tanzania mjini hapa. Twanga Pepeta katika picha ya pamoja na viongozi

Cllub 2000 palikua hapatoshi

Akiwakaribisha wote Balozi Kallaghe alisema sherehe za miaka 50 ni idhinisho kuwa Tanzania ni nchi ya amani inayostahili kuwa fahari yetu sote. “Waangalie Waingereza wanavyoorodhesha tarehe na mida ya majengo yao muhimu. Kutambua na kusherehekea muda kamili wa matukio ya jamii ni jambo muhimu na la kawaida,” alikumbusha kiongozi huyo na kupigiwa makofi.

Muda wa kusugua visigino

Makamuzi yakiendelea

Sekta ya kukaanga chips..Kikazi zaidi

Mh Balozi na Mama Balozi wakifungua mziki

Mh Chabaka na Mchumba wake wakicheza

Twanga wakifanya kweli

Kila mtu akifurahia show ya twanga

Na Freddy Macha
Watanzania wa kila rika, nasaba na taaluma walifurika toka miji ya Leeds, Bristol, Birmingham, Northampton, Milton Keynes na vitongoji mbalimbali kufurahia vigongo vya bendi hili lenye makao makuu Mango, Kinondoni Dar es Salaam. Ukumbi wa Club 2000 Banqueting Suite ulioko nyuma ya uwanja maarufu wa Wembley ulishuhudia tafrija hiyo wakati viongozi rasmi wa serikali walipofungua tafrija wakicheza nyimbo maarufu za Kitanzania kama ule wa mwanamuziki Salum Abdallah (“Wanawake wa Tanzania” na “Tujenge Nchi Yetu”) marehemu alizoimba mara baada ya Uhuru mwaka 1961.

Viongozi waliojumuika walikuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na serikali za mitaa, Mheshimiwa Aggrey Mwanri, Balozi wetu Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe, naibu wake Mheshimiwa Chabaka Kilumanga na Ofisa Habari ndani ya ubalozi,Mheshimiwa Amos Msanjila aliyehamasisha wageni kwa kunyofoa kinywaji cha “champagne” mahsusi kuzindua maadhimisho.

Kutokana na maombi mengi ya washabiki Twanga Pepeta itafanya Show ya pili siku ijumaa Tarehe 2 Desemba 2011 katika mji wa Milton Keynes kwenye ukumbi wa Golden Lounge, Unit 35 Barton Road, Bletchley Milton Keynes. MK2 3UH

Show hii imeandaliwa na Urban Pulse wakishirikiana na Miss Jestina blog.