Monday, November 28, 2011

TWANGA PEPETA YADONDOSHA MAKOMBORA KUAMSHA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU LONDON

African Stars Entertainment Tanzania(Aset) ambao wanajulikana kwa jina la “Twanga Pepeta” walikuwa kivutio cha sherehe za miaka 50 ya Uhuru London juzi Jumamosi. Kikosi hiki cha watumbuizaji maarufu wa Kibongo kilikaribishwa na Urban Pulse, Jestina George wakishirikiana na Ubalozi wa Tanzania mjini hapa. Twanga Pepeta katika picha ya pamoja na viongozi

Cllub 2000 palikua hapatoshi

Akiwakaribisha wote Balozi Kallaghe alisema sherehe za miaka 50 ni idhinisho kuwa Tanzania ni nchi ya amani inayostahili kuwa fahari yetu sote. “Waangalie Waingereza wanavyoorodhesha tarehe na mida ya majengo yao muhimu. Kutambua na kusherehekea muda kamili wa matukio ya jamii ni jambo muhimu na la kawaida,” alikumbusha kiongozi huyo na kupigiwa makofi.

Muda wa kusugua visigino

Makamuzi yakiendelea

Sekta ya kukaanga chips..Kikazi zaidi

Mh Balozi na Mama Balozi wakifungua mziki

Mh Chabaka na Mchumba wake wakicheza

Twanga wakifanya kweli

Kila mtu akifurahia show ya twanga

Na Freddy Macha
Watanzania wa kila rika, nasaba na taaluma walifurika toka miji ya Leeds, Bristol, Birmingham, Northampton, Milton Keynes na vitongoji mbalimbali kufurahia vigongo vya bendi hili lenye makao makuu Mango, Kinondoni Dar es Salaam. Ukumbi wa Club 2000 Banqueting Suite ulioko nyuma ya uwanja maarufu wa Wembley ulishuhudia tafrija hiyo wakati viongozi rasmi wa serikali walipofungua tafrija wakicheza nyimbo maarufu za Kitanzania kama ule wa mwanamuziki Salum Abdallah (“Wanawake wa Tanzania” na “Tujenge Nchi Yetu”) marehemu alizoimba mara baada ya Uhuru mwaka 1961.

Viongozi waliojumuika walikuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na serikali za mitaa, Mheshimiwa Aggrey Mwanri, Balozi wetu Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe, naibu wake Mheshimiwa Chabaka Kilumanga na Ofisa Habari ndani ya ubalozi,Mheshimiwa Amos Msanjila aliyehamasisha wageni kwa kunyofoa kinywaji cha “champagne” mahsusi kuzindua maadhimisho.

Kutokana na maombi mengi ya washabiki Twanga Pepeta itafanya Show ya pili siku ijumaa Tarehe 2 Desemba 2011 katika mji wa Milton Keynes kwenye ukumbi wa Golden Lounge, Unit 35 Barton Road, Bletchley Milton Keynes. MK2 3UH

Show hii imeandaliwa na Urban Pulse wakishirikiana na Miss Jestina blog.

Sunday, November 27, 2011

BURUDANI YA ST8 MUZIK NDANI YA LEADERS 2011

Mwanamuziki wa hip hop toka nchini Marekani Fabolous akikamua kwenye tamasha hilo lililo hapen katika viwanja vya Leaders jijini Dar na kuhudhuriwa na bonge la nyomi

Fasi ya mbele na maburudanizzz.

Msanii wa Hip hop toka bongo land Jay Mo akikamua sanjari na mwana hip hop mwenzie Mchizi Mox

Ze nyomiz.

Simba mzee, Mfalme asiyevuliwa taji Selemani Msindi aka Afande Sele alikosha kisasawa mashabiki walo hudhuria tamasha hilo.

Masoja Long time kitambo wanaitwa Gangwe Mobb.

Flash ze nyomi.

C it again n again.
Picha zote na MICHUZIjr

MITINDO YA HOME YATINGISHA MARYLAND US


Picha zote na (Swahilivilla Abou Sharty)
http://swahilivilla.blogspot.com/

JOSE CHAMELEONE AWARUSHA WAKAZI WA DMV

Ilikuwa ni Jumatano Nov23, 2011 katika sherehe za Thanksgiving nchini Marekani ambapo muimbaji Jose Chameleone toka nchini Uganda alikamua.

Mamia ya watu walifurika kuja kumuangali Msanii huyo toka Nchini Uganda kwa jina maarufu la Jose Chameleone, ana nyimbo zake, ikiwemo Mama roda, Jamila analia, na nyingi nyingi.

Muziki unaponoga warembo mikono juuuu!!!

Wakati mwingine warembo hupandwa na jazba ya maraha na kwa wale wanaoshindwa kujizuia hukinasa kinasa ili wapate chombeza, hapa ni mdafada akichombeza kwenye songi la 'kipepeo'.

Mambo ya utamuZz hayo cheza ni kuchezee ndani ya Rendezvous Hall nchini marekani.

Wanasema muziki wako ukikubalika kwa warembo baaaasi umewini! chekshia mahudhurio.

Aj Ubao alikuwa ni mwimbaji wa pili kuimba katika onyesho hapa ni nyuma ya jukwaa akipata flash ya pamoja na mdhamini wake wapendo.

Muimbaji Ana Lov akipata flash ya pamoja na rafiki yake kwenye onesho hilo la Mwanamuziki wa Uganda Jose Chameleone.

WadadaZzzz.warembo.com ndani ya ukumbi wa Rendezvous mitaa ya Parklawn Dr, Rockville Maryland U.S

Nyuma ya jukwaa mwanadada Luren akipata flash.

Cheza ni kuchezee na flash!!!

Mwana muziki wa kizazi kimpya ndani ya Washington DC, AJ Ubao wa kwanza (kushoto) pamoja mzee wa kuwachanganya Dmk global Dickson Mkama, wa kwanza( kulia) wakiwa nyuma ya jukwaa na Jose chameleone aliyekuwa akisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa muziki wake.

Picha zote na http://swahilivilla.blogspot.com