Wednesday, June 27, 2012

HAPPY BIRTHDAY CUTHBERT A. G. SENGO


Miaka minne iliyopita Siku kama ya leo my son Cuthbert anazaliwa akitofautiana wiki tu na tarehe ya kaka yake.
Happy Birthday to you my kid n' I wish all the best.
Papa & mama love's U'

WEMA SEPETU AZINDUA FILAMU YAKE 'SUPER STAR'



Wema Sepetu akipozi kwa picha mara baada ya kukaa kabla ya kuanza kuchezwa kwa Demo ya filamu hiyo usiku huu kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro.


Wageni waalikwa mbalimbali wakishuhudia uzinduzi wa filamu ya Super Star iliyochezwa na mwana dada Wema Sepetu kwenye hotli ya Hyyat Kilimanjaro


Hali ukumbini wakati wa uzinduzi wa filamu Super Star ya Wema Sepetu aliyoizindua kwenye hotel ya Hyyat Kilimanjaro jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo ikihudhuriwa na watu maarufu pamoja na wanamuziki na waigizaji.

Mtangazaji wa XXL B12 na friendz

Kutoka shoto ni Mange Kimambi, Wema Sepetu na Miriam Odemba

Omotola na makaribisho ya burudani.
Wanamzuiki, watangazaji pamoja na waigizaji mbalimbali wa filamu walihudhuria katika uzinduzi huo kutoka kulia ni Charles Baba wa Mashujaa Band, Hatman, Mtangazaji Benny Kinyaiya, Mchekeshaji Steve Nyerere, Muigizaj Ramond Kigosi, mwanamuziki Barnaba na Richie Mtambalike "Rich Rich" wakishoo Love.
Mwanamuziki Mwinyi ambaye ndiye aliyemvisha pete ya Uchumba Wema Sepetu katika filamu hiyo naye alikuwepo kwenye uzinduzi huo.

The area
Waigizaji mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo
Kundi la THT likifanya vitu vyake katika uzinduzi huo
Ankal Michuzi na maiwaifu wake kulia na rafiki yao wakipozi kwa picha

Kutoka kulia ni Asma Makau, Dina Marios, Moonshine na Janet wakiwa katika pozi kwenye uzinduzi huo.

Tuesday, June 12, 2012

MAKAMUZI YA MACHOZI BAND NA BARNABA YALIVYOFANA ROCK CITY

Video ya mduara wa Machozi Band.



Langoni ilikuwa unakutana na CD original za Lady jay Dee na Machozi Band
 

Ze dadaz wakipata flash juu ya red carpet kabla ya kuingia ukumbini, katikati ni Rhoda John, Asha Kissy na mashost zao...
 
  Kutana na Blogger Allan Kisoi pale kati akipata flash na Antonio Nuggas, Barnaba na Hellen.
  
Machozi Band katika Stage la Gold Crest Manza.

 Mc wa shughuli usiku huo Albert G. Sengo toka Clouds Fm 88.1 Mwanza

 
Dance la Machozi Band likiendelea.
Mduara na mauno yamekolea anatunukishwa mtu kitu cha msimbazi.

Mikono kwenye pembejeo na zana maho kwenye kamera na Machozi Band.

Mwimbaji mwenye umri mdogo kuliko wote hatari kwenye stage Sam Machozi.

Sutumuka ya kwaitoZZZZzzz.com

Dance la kwaito.

Barnaba alichengua vilivyo.

Hadi ladiZ wanakiri kuwa Barnaba ni 'moTTo'

Nishakwambia kuwa Barnaba ni 'Motto' 

Mwanamuziki haitwi 'Mwanamuziki' bila kujua kutumia japo chombo kimoja wapo cha muziki.


Wageni toka mbali hawakukosa.

Kutoka kulia Anthonio Nuggaz wa Kambi popote, Captein Gadna G. Habbash, Ramma wa Villa Park na Albert G. Sengo

Zungusha zungusha....

PICHA LINAENDELEA...

Monday, June 11, 2012

MPAMBANO KATI YA MSONDO NA SIKINDE KUSINDIKIZA SHEREHE ZA VILLA PARK KUTIMIZA MIAKA MITANO

Villa Park Resort Mwanza inaadhimisha miaka mitani tangu kuanzishwa kwake, shamrashamra zitaanza wiki hii siku ya alhamisi katika usiku wa Mwambao ambapo mwanamama Jokha Kassimu atatoa burudani akichagizwa na Kanga Moko Ndembendembe kwa kiingilio cha sh 3000/=


Vilevile kwa mujibu wa mratibu mkuu wa soka Mzee Halphan Ngasa amesema kuwa kutakuwa na ligi ya mtoano (Villa Soccer Bonanza) ambapo timu za Mashabiki na wafanyakazi za Villa Sports Club, Lakairo Sports Club, Victoria Sports Club na Shooters Sports Club zitachuana.


Mshindi wa kwanza kwenye ligi hiyo ya mtoano kupata kombe kubwa, mbuzi na kreti ya kinywaji kutoka wadahamini TBL, mshindi wa pili kunyakuwa kombe na kreti mbili za kinywaji toka TBL, mshindi wa tatu ataondoka na kombe na kreti moja ya kinywa cha TBL


Lengo la mashindano hayo ni kuboresha afya na kusisitiza umuhimu wa mazoezi kwa jamii hususani watu wazima.

Burudani nyingine siku ya Ijumaa katika Compass Night na Miaka mitano ya Villa Park Dj PQ (Clouds fm) na Dj Mafuvu (East Africa Radio) na maDj wote wa Villa Park (Dj John Lyatow, Dj Samm, Dj Chriss) kumwaga burudani usiku huo kiushindani zaidi.

Katika usiku  wa Jumamosi Sambamba na disco kali ndani ya Villa Disco Teque vilevile uwanja wa nje kutakuwa na mpambano awamu ya kwanza wa Bendi za Msondo, Sikinde na bendi ya jijini Mwanza Super Kamanyola kiingilio usiku huo shilingi 5,000/= na shilingi 7,000/= kuzama hadi ndani.


Jumapili kuanzia saa 12 jioni ni Mpambano wa kukata na Shoka kati ya Bendi tatu kongwe hapa nchini zenye mashabiki wengi kama Simba na Yanga nazungumzia Msondo, Sikinde na Super Kamanyola nani zaidi?