Sunday, June 29, 2014

LULU, MILARD AYO, KING MAJUTO WAIBUKA VINARA KATIKA SHEREHE ZA UTOAJI TUZO ZA WATU KATIKA HOTELI YA SERENA

Burudani ikiendelea ndani ya Ukumbi uliopo Serena Hotel katika sherehe za utoaji wa Tuzo za watu
Wadau wakifuatilia Tuzo za Watu
Jimmy Kabwe akiendelea Kutangaza
 Meneja Masoko wa Kampuni ya Proin Promotions Limited, Evance Stephen (Kushoto) akiwa na Msanii Bora wa Kike katika Tuzo za Watu Elizabeth Michael maarufu kama Lulu mara baada ya Kutangazwa Mshindi wa Kipengele cha  Msanii Bora wa Kike anayependwa.
 Salama Jabir akiiwa juu ya Steji kwaajili ya kukabidhi tuzo ya Muongozaji Bora wa Video anayependwa
 Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili Kutoka BBC Salim Kikeke akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa wadau wake
 Faraja Kota Nyalandu (Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mrs Mengi Kylin
 Wakurugenzi wa Bongo 5
 Babu Tale akipokea tuzo ya Video bora Kwa Niaba ya Msanii Diamond Ambae hakuwepo katika Utoaji Tuzo hizo. Nyimbo ya My Number one ya Diamond Ndio Nyimbo inayopendwa
 Mustafa Hassanali (Kulia) akimkabidhi Mwakilishi wa Lady Jay Dee Tuzo ya Video Bora ya Yahaya
Wadau wakifuatilia Sherehe za Utoaji Tuzo hizo zilizofanyika jana katika Ukumbi uliopo katika hoteli ya Serena
 Watangazaji wa Clouds Media , Adam, Millard Ayo na B12 wakijadiliana jambo wakati wa sherehe za utoaji tuzo za Watu.
 Millard Ayo akipokea Tuzo ya Mtangazaji wa Radio wa kiume anayependwa mara baada ya kuibuka mshindi katika kipengele hiko
 Akiwashukuru Wadau waliompigia kura na kumpa sapoti
 Salim Kikeke kutoka Idhaa ya Kiswahili ya BBC akiwashukuru wadau wake waliomuwezesha kushinda Tuzo 
King Majuto akifurahi mara baada ya kuppokea Tuzo yake mara baada ya kutangazwa mshindi wa Kipengele cha Msanii Bora anayependwa wa Kiume.Picha Zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

Monday, June 16, 2014

HIVI NDIVYO VUNJA JUNGU LA MWANZA LITAKAVYO KUWA...!!

Vunja jungu 2014 safari hii Villa Park inakuletea Mkali Nani kati ya Bendi mbili za kisasa Bodaboda Band ya mwanamuziki Kidumu toka nchini Kenya na Malaika Band yake Cristian Bella toka nchini Tanzania.
Ni Ijumaa 27/06/2014.
 ....Unakosaje??....!!!

HIZI HAPA PICHA ZA NDOVU PARTY.

Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli  na Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Nchini(TBL) wakionyesha Kikombe walichoshinda kupitia bia ya Ndovu kutoka katika Kampuni ya Kimataifa ya Monde Selection nchini Ufaransa kama bia  yenye ubora wa kimataifa wakati wa hafla ya kupongezanma na wadau wa bia hiyo iliyofanyika Dar es Slaam jana.
Kundi la wasanii wa THT wakitumbuiza wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Masoko TBL,Kushila  na Meneja masoko TBL, Fimbo Butallah wakizungumza na wadau.
Meneja masoko TBL, Fimbo Butallah na Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt wakiteta jambo.
Wadau wa Bia ya Ndovu Special Malt wakigonganisha glasi wakati wa hafla hiyo.
Mwanamuziki, Halima Mdee akitumbuiza wakati wa hafla ya kujipongoza kwa wadau wa bia ya Ndovu Special Malt mara baada ya bia hiyo kushinda tuzo ya Ubora wa Kimataifakutoka katika Taasisi ya Kimataifa ya Monde Selection iliyofanyika katika Hotel ya Hayati Kilimanjaro Dar es Salaam.
Msanii wa nyimbo za kizaji kipya , Halima Mdee akitumbuiza wakati wa hafla ya kujipongoza kwa wadau wa bia ya Ndovu Special Malt mara baada ya bia hiyo kushinda tuzo ya Ubora wa Kimataifakutoka katika Taasisi ya Kimataifa ya Monde Selection iliyofanyika katika Hotel ya Hayati Kilimanjaro Dar es Salaam.
Wadau wakiwa katika hafla hiyo.
Wadau wa meza hii.
Sisters wakiwa katika hafla hiyo.
Wadau wakiwa katika hafla hiyo.