Sunday, July 19, 2015

VIJANA CCM WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHUKUA FOMU ZA UBUNGE JIMBO LA MOSHI MJINI

Mtia nia wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini,Priscus Tarimo,akikabidhiwa fomu ya nafasi hiyo na katibu wa CCM manispaa ya Moshi,Loth Ole Nesele katika ofis za chama hicho za Wilaya ya Moshi mjini.
Mtia nia ya kugombea Ubunge jimbo la Moshi mjini,Priscus Tarimo,akitoa maelezo yake kwa Katibu Msaidizi wa CCM wilaya ya Moshi mjini Donatha Mushi alipofika kwa ajili ya zoezi la uchukuaji wa fomu.
Priscus Tarimo akizungumza na na wanahabari( hawako pichani) muda mfupi baada ya kumaliza zoezi la uchukuaji wa fomu za kuwania kuteuliwa katika nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM jimbo la Moshi mjini.
Naibu kamanda wa Vijana wa CCM,manispaa ya Moshi ,Edmund Rutaraka akipokea fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho kutoka kwa katibu msaidizi wa CCM wilaya ya Moshi mjini,Donatha Mushi.
Kada wa Chama cha Mapinduzi manispaa ya Moshi ,Daudi Mrindoko akiwa ameambatana na mkewemalipofika kucukua fomu katika ofisi za CCM wilaya ya Moshi mjin,Fomu hizo zilikabidhiwa kwake na katibu msaidizi wa chama hicho Donatha Mushi.
Mwakilishi wa jamii ya Bantu Union ,Omary Mwaliko akirejesha fomu za kuwania kuteuliwa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini mara baada ya kuzijaza

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WAKAZI WA JIJI LA MWANZA WAJITOKEZA KUMLAKI KWA SHANGWE DKT MAGUFULI JIJINI MWANZA JANA

 Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia Wananchi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kwa wingi jioni ya jana.
Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake,nje ya ofisi za CCM mkoa,ambao walijotokeza kumlaki kwa shange na furaha kubwa.Dkt Magufuli amewasili jana jijini Mwanza akitokea jijini Dar kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na wananchi kwa ujumla.

 Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi alipokuwa akiwasili jijini Mwanza jioni ya leo akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa juu wa chama cha CCM,Magufuli yuko jijini Mwanza kujitambulisha kwa Wananchi.
 Mke wa Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi Dkt.John Pombe Magufuli,Mama Janeth Magufuli akiwasalimia Wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake waliojiotokeza kwa wingi kuwapokea,Pichani kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye. 
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake,nje ya ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.

 Baadhi ya Wananchi wakilikimbiza gari la  Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli kwa shangwe kama waonekanavyo pichani ,wakati Magufuli lipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 Baadhi ya Wananchi wa jiji la Mwanza wakiwa wamefunga barabara kwa muda wakishangilia ujio wa  Mgombea Uraisi wa CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 kuna wengine waliacha kazi kwa muda kama hizi na kuja kwenda kushangilia ujio wa Mh.Dkt John Magufuli
  Wananchi wa Passians wakimpokea na kumshangila Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 Baadhi ya Wanahabari wakiwa kazini.
  Wananchi wa eneo la kona ya Bwiru wakiwa wamezuia  msafara wa Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla.
 Wananchi wa eneo la kona ya Bwiru wakiwa wamezuia  msafara wa Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla.
    Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh.Magesse Mulongo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa jiji hilo,kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu.
    Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Mh John Monela mara baada ya katika uwanja wa ndege wa jiji la Mwanza.
   Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alisalimiana na wafuasi wa chama hicho wakiwemo viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza,alipowasili katika uwanja wa ndege wa jiji hilo.

Friday, July 17, 2015

AMINI SALIMINI AWANIA UBUNGEA JIMBO LA MKWAJUNI ZANZIBAR KUPITIA TIKETI YA CCM

Mtoto wa Komando Dk Salmin Amour Juma Amini Salimini achukua Fomu kogombea Jimbo la Mkwajuni Zanzibar akiwasili katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kaskazini A Gamba kwa ajili ya kuchukua Fomu kogombea Jimbo hilo, akisalimiana na Wananchi waliopo hapo. 
Mama wa Amini Salimi Bi Khadija Kasimi akisalimiana na Katibu Msaidi wa Ofisi ya CCM Wilaya Kaskazini A Unguja alipofika katika Ofisi hizo kumshindikiza Mtoto wake kuchukua Fomu ya Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni Zanzibar. 
Katibu Msaidizi wa Ofisi ya CCM Wilaya ya Kaskazini Unguja Ndg Shafi Hamad akitowa maelezo kwa Mgombea kabla ya kumkabidhi fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea Jimbo la Mkwajuni
Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni Amini Salimini akihesabu fedha kwa ajili ya kulipia Fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Ubunge kupitia CCM katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kaskazini Unguja Gamba.
Katibu Msaidi Ofisi ya CCM Wilaya ya Kaskazini a Unguja Ndg Shafi Hamad akimkabidhi Fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Mkwajuni Amini Salimini, baada ya kukamilisha taratibu zote za malipo na kutimiza masharti ya Chama cha Mapinduzi.
Katibu Msaidi wa CCM Wilaya ya Kaskazini A Unguja akitowa maelezo kwa mgombea baada ya kumkabidhi fomu hiyo Ndg Amini Salimini.
Mgombea wa Jimbo la Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini A Unguja  Amini Salimini akiwa katika picha ya kumbukumbu na familia yake baada ya kuchukua Fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni kwa tiketi ya CCM, akiwa katika Ofisi za CCM Gamba.
Amini Salimini akiwa katika picha ya pamoja na familia yake baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mkwajuni Zanzibar.Akionesha fomu yake baada ya kukabidhiwa kwa hutua za ujazaji 
Amini Salimini akitoka katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kaskazini A Unguja baada ya kuchukua fomu hiyo akionesha kwa wananchi walioko katika eneo hilo.
Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini A Unguja Amini Salimini akiwa na Mtoto wake wa Kwanza wakishikilia fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuiwakilisha CCM katika Jimbo la Mkwajuni Zanzibar. 
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni Amani Salimini akiomba dua katika makaburi ya Wazee wake huko Kidombo baada ya kuchukua Fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Mkwajuni Zanzibar
Amini Salimini akipata dua kutoka kwa Wazee wa Kijiji cha Kidombo Mkwajuni baada ya kuchukua Fomu ya Kugombea Ubunge wa Jimbu la Mkwajuni Zanzibar kupitia CCM

BI. CHIKULUPI NJELU KASAKA ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE WA VITI MAALUM,VIJANA -MBEYA ,ATOA VIPAUMBELE VYAKE.

Bi. Chikulupi Njelu Kasaka 
Mgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Mbeya Bi. Chikulupi Njelu Kasaka (Kushoto) akikabidhiwa Fomu ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana Mbeya na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Bi. Aida Mamu
 Kushoto ni Bw. Moses Mwakibinga Katibu wa Hamasa na Chipukizi Wilaya ya Chunya, Bi. Chikulupi Njelu Kasaka (Kushoto)  na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Bi. Aida Mamu Baada ya kukabidhiwa Fomu

                  MFAHAMU BI. CHIKULUPI NJELU KASAKA

*Anaitwa Chikulupi Njelu Kasaka.

*Ni Mwanasheria (wakili) kitaaluma.


*Ni mfanyakazi wa Bunge la JMT
.
*Sasa anawania Ubunge wa Viti-maalum (vijana).


*WASIFU WA MGOMBEA: BI. CHIKULUPI KASAKA

ELIMU:
Chikulupi Kasaka ni mzaliwa wa Chunya na babu na Bibi ni wakazi wa Kijiji cha Mtanila katika Wilaya ya Chunya.

 Chikulupi alizaliwa mwaka 1986 na kuanza elimu ya msingi mwaka 1994 katika shule ya Chunya Kati. Chikulupi alimaliza elimu ya msingi Mkoani Tabora na kuchaguliwa kwenda shule ya Serikali ya Sekondari ya Wasichana Msalato iliyopo Dodoma ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha nne mwaka 2000-2004. Mwaka 2005-2007 alijiunga na Shule ya Serikali ya Sekondari ya Wasichana Loleza iliyopo Mkoani Mbeya. Alishaguliwa kijunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2007 kusomea Shahada ya Kwanza ya Sheria na kumaliza mwaka 2011. Mwaka 2013 alijiendeleza kwa kujiunga na mafunzo ya uanasheria kwa vitendo na kumaliza mwaka 2014 katika chuo kiitwacho Law School of Tanzania ambapo baadaye niliapishwa kuwa wakili.

UZOEFU KATIKA UONGOZI:
Chikulupi aliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi akiwa anasoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Alikuwa Mbunge katika Serikali ya wanafunzi - DARUSO.

 Chikulupi alichaguliwa mwaka 2009 kuwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Wanafunzi wa Afrika Mashariki uitwao East Africa Community Students Union -EACSU.

 Pia alikuwa Afisa Mahusiano ya Umma katika Taasisi ya wanafunzi wa Sheria iitwayo University of Dar es Salaam Human Rights Association –UDHRA. Mwaka 2010 alishiriki mafunzo ya Uongozi kwa Vijana yaliyofadhiliwa na Shirika la Kijeruman liitwalo Friedrich Ebert Stiftung –FES.

 Pia mwaka 2014 alishiriki mafunzo ya Viongozi Vijana toka barani Afrika nchini Marekani ambao alisomea masomo ya Public Management katika chuo cha Howard kilichopo Washington. Pia nilipata fursa ya kukutana na Rais Barack Obama ambae ni mwanzilishi wa mafunzo haya.

UZOEFU NDANI YA CHAMA/UVCCM:
Chikulupi Kasaka alijiunga na CCM hasa katika jumuiya ya UVCCM mara tu baada ya kumaliza elimu ya sekondari 2006. 
Alipokuwa anasomea Shahada ya Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alijikita katika shughuli mbalimbali za kuimarisha chama na mwaka 2010 alichaguliwa Mwenyekiti wa UVCCM tawi ya Abiyan-Chuo Kikuu. Na mjumbe wa Shirikisho la Vyuo Vikuu wanaCCM, Mkoa wa Dar es Salaam.

KAZI:
Mara baada ya kumaliza chuo kikuu Julai 2011 Chikulupi alifanya kazi katika Shirika la Wakimbizi katika Mradi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam uitwao International Migration Management Program (IMMP). 

Mwaka 2012 aliajiriwa na Serikali kama Hakimu Mkazi daraja 2, katika Mahakama ya Mwanzo Makongorosi-Chunya, Mbeya. Mwishoni mwa mwaka 2012 nilijiunga na utumishi wa Chama Makao Makuu ya CCM Dodoma. 

Nilipangiwa kufanya kazi za Chama katika Upande wa Bunge hasa za kisheria. Tangu kipindi hicho mpaka sasa Chikulupi anafanya kazi kama Msaidizi wa Katibu wa Wabunge wote wa CCM, Bungeni Dodoma.

VIPAUMBELE:
Chikulupi Kasaka anaomba ridhaa yako ili aweze kuwawakilisha vijana wa Mkoa wa Mbeya katika nafasi ya Uongozi wa Kitaifa kupitia ngazi ya Ubunge wa Viti Maalum-Vijana. 

Kama mkazi wa Mbeya naamini vijana wa Mbeya wanauwezo, nguvu, bidii na jitihada katika shughuli zao za kila siku. Lakini mimi nitapigania kuwapatia vijana wa Mbeya fursa nyingi zaidi katika vipaumbele vifuatavyo: 

ELIMU, AJIRA, MICHEZO, UTALII na AFYA.
ANAOMBA UMUUNGE MKONO KWA FURSA ZAIDI KWA VIJANA WA MKOA WETU WA MBEYA.



MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MBAGALA MWINCHUM ACHUKUWA FOMU

Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbagala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mwinchum Msomi  akisalimiana na mgombea Ubunge kupiti chama hicho Dk. Faustine Ndugulile anaye tetea Jimbo lake walipokutana Ofisi za chama hicho Wilayani  Temeke Dar es Salaam jana (PICHA NA KHAMISI MUSSA)
Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbagala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mwinchum Msomi, akimkabidhi Pesa  Katibu Umoja wa Vijana Wilaya ya Temeke Yona Sengerema , kwaajili ya malipo ya uchukuaji wa  fomu.
 Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbagala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mwinchum Msomi, akisaini fomu mbalimbali mbele ya   Katibu Umoja wa Vijana Wilaya ya Temeke Yona Sengerema.

Katibu wa Umoja wa Vijana wilaya ya temeke akimkabidhi Fomu  Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbagala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mwinchum Msomi alipofika ofisini hapo Dar es Salaam jana kuchukua fomu hizo.

Thursday, July 16, 2015

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BAGAMOYO ACHUKUA FOMU WENGI WAMPONGEZA


 Mgombea Ubunge Jimbo la Bagamoyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mathew Juma Salum Yungwe, akionesha fomu ya kugombea nafasi hiyo baada ya kukabidhiwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Bagamoyo, Kombo Kamote wilayani humo leo mchana.
 Katibu Msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bagamoyo, Salum Mtelela (kulia), akimkabidhi stakabadhi ya malipo ya kuchukua fomu, Mgombea huyo.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Bagamoyo, Kombo Kamote (kushoto), akimkabidhi fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Bagamoyo, Mathew Juma Salum Yungwe wilayani humo leo mchana. Wa pili kulia ni Mama mzazi wa mgombea, Mary Yungwe na Meneja wa Kampeni wa mgombea huyo, James Mbuligwe.
 Hapa mgombea huyo Mathew Yungwe, akionesha fomu hiyo baada ya kukabidhiwa.
 Makada wa CCM wakimpongeza Mgombea huyo wakati wa kuchukua fomu hiyo.
 Mgombea nafasi hiyo ya Ubungo Jimbo la Bagamoyo, Mathew Yungwe (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na mama yake Mary Yungwe (kulia) na Meneja wa Kampeni wake, James Mbuligwe.
Hapa mgombea huyo na mama yake na meneja kampeni wake wakiondoka ofisi ya CCM Wilaya ya Bagamoyo baada ya kukabidhiwa fomu yake. 

Wednesday, July 15, 2015

JUMAA MHINA 'PIJEI' ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KAWE, ATAJA VIPAUMBELE VYAKE

Hapa ikionesha fomu baada ya kukabidhiwa.
 Kada wa CCM Jumaa Mhina 'Pijei' (katikati), akipokea fomu ya kuwania ubunge Jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam, kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe leo mchana. Anaye shuhudia kulia ni Kada wa chama hicho anayewania ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia CCM, Ramadhan Ndanga 'Potipoti'.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimpa maelezo ya kufuata baada ya kukabidhiwa fomu hizo.
Waandishi wa habari wakimuhoji nini atawafanyia wananchi wa Jimbo la Kawe iwapo atachaguliwa.

Na Mwandishi Wetu

MUWANIA nafasi ya Ubunge Jimbo la Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumaa Mhina 'Pijei' amesema akipata nafasi hiyo atashirikiana na wananchi wa jimbo hilo katika kutatua changamoto zilizopo.


Hayo aliyasema wakati akichukua fomu ya kugombea nafasi hiyo Dar es Salaam leo mchana na utaja vipaumbele vyake vya maendeleo atakayofanya.

Alisema mwaka 2010 aligombea lakini katika kura za maoni ya ccm hazikutosha, mwaka huu anaamini zitatosha na kulikomboa jimbo lililo mikononi mwa wapinzani.

Alisema kipaumbele chake ni ajira kwa vijana, elimu, miundimbinu ya barabara na umeme na kuwa mafanikio hayo yatakuja iwapo atashirikiana kwa karibu na wananchi hivyo aliomba wananchi kuto muangusha wakati ukifika.

Alisema tayari ametoa ajira kwa vijana kwa kuwapa bodaboda ambazo zimepunguza tatizo la ajira na vitendo vya uhalifu katika jimbo hilo.

Mhina alisema kipaumbele kingine atakacho kitoa ni kuhakikisha anatumia uzoefu wake wa ujasiriamali kwa kuwajengea uwezo wanawake na vijana kwa kuwapa elimu na kuwawezesha kupata mikopo yenye riba nafuu ili kuinua mitaji yao.