Thursday, April 12, 2012

MWANZA YATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU JENERALI MSTAAFU

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. Ernest Ndikilo leo ameongoza Umma aliojitokeza kutoa salamu za rambirambi kwa mwili wa aliyewahi kuwa mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro aliyefariki dunia siku ya Jumanne wiki hii akiwa na umri wa miaka 87 ambaye ameagwa rasmi leo jijini Mwanza.
Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro alizaliwa mnamo tarehe 1/01/1923 nakufariki dunia 10/04/2012.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ernest Ndikiro akimfariji mke mdogo wa marehemu Zainab Kiaro.
Mmoja wa wanafamilia (Kushoto) akimfariji mke wa kwanza wa marehemu Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro aitwaye Penina Kiaro (Kulia).
Makamanda wakijadiliana.
Makamanda wakizidi kufurika eneo la tukio kutoa salamu zao za mwisho kwa mwili wa marehemu.
Makamanda wakiwa eneo la juu katika kilima kidogo cha mawe ili kushuhudia ibada ya salamu za mwisho jijini Mwanza.
Safu ya Makamanda wengine.
Mwili huo ulitoka katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando mchana na hatimaye majira ya saa saba ukaagwa hapa katika nyumba yake ya kikazi maeneo ya Kapripoint kabla ya kusafirishwa kuelekea wilayani Tarime mkoani Mara kwaajili ya Mazishi.
Kwa mwendo wa pole mwili ulipelekwa eneo rasmi.
Moja kati ya wanajeshi akiongoza moja ya vifungu kwenye ibada hiyo.
Mapaparazi.
Wakati wa kutoa heshima za mwisho uliwadia.
Jeshi la polisi usalama barabarani nao walikuwepo kutoa heshima zao.
Heshima...
Heshima ziliendelea kutolewa.
Makamanda wakipanga mikakati.
Mzee Gachuma katikati akifanya majadiliano na baadhi ya maafisa wa Jeshi.
Msafara.
Mwili wa marehemu aliye kuwa mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro umesafirishwa leo kuelekea wilayani Tarime mkoani Mara kwaajili ya Mazishi ambayo yatafanyika kesho.

No comments:

Post a Comment