Showing posts with label HUZUNI. Show all posts
Showing posts with label HUZUNI. Show all posts

Sunday, July 14, 2013

MBUNGE WA MUSOMA MJINI PAMOJA NA MEYA WASHIRIKI MAZISHI YA HUPHREY SIMON MKOANI MARA

Padre akiongoza ibada kumuombea marehemu Humphrey Simon iliyofanyika jana nyumbani kwao Makoko Musoma mjini. 

Mbunge wa Musoma mjini Mhe. Vicent Nyerere (katikati mwenye suti nyeusi) alihudhuria ibada hiyo sambamba na mazishi.

Waumini walishiriki meza ya bwana katika ibada hiyo ya kumuombea marehemu.

Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisusura akishiriki meza ya bwana.

Mmoja ya viongozi wa kampuni ya mawasiliano ya tigo akishiriki meza ya bwana.

Kusanyiko kwenye ibada nyumbani.

Mama Nyimbo akiongoza safu ya akinamama wenzake katika utoaji heshima za mwisho kwa mwili wamarehemu.

Sambamba wananchi wengine Mbunge wa Musoma Mjini Vicent Nyerere akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.

Mashangazi na ndugu wa karibu wa marehemu wakitoa heshima za mwisho 

Heshima za mwisho zilikoma kwa safu ya wanaume kufunga zoezi hilo.

Kisha safari ya kuelekea makaburini eneo la Makoko Musoma mkoani Mara ikafanyika.

Wafanyakazi wa Kampuni ya Tigo ambao wanafanya kazi na mke wa marehemu walitoa sapoti ya kutosha katika shughuli nzima za mazishi, hata wengine walidiriki kusafiri toka mikoa mbalimbali ili kuwakilisha.

Mwili wa marehemu Huphrey Simon ukiwa kwenye nyumba yake ya milele.

"Uliumbwa kwa udongo na mavumbini utarudi"

Mke wa marehemu Bi. Neema akiweka udongo kwenye kaburi la mumewe.

Mke wamarehemu akiweka shada la maua.

Mjomba wa marehemu Mr. Tega akiwa na shangazi wakiweka shada la maua.

Shangazi wa marehemu.

Mbunge wa Musoma mjini Mhe. Vicent Nyerere akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Humphrey.

Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisusura akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Humphrey.


Mtoto wa marehemu akiweka shada la maua. 
Picha ya pamoja ya wanandugu akiwepo mke wa marehemu (wa 3 kutoka kushoto) mbele ya kaburi .

Mtoto wa marehemu Huphrey Simon akiweka shada la maua juu ya kaburi la baba yake.

Marafiki wa marehemu.

Jina la bwana lihimidiwe.

Thursday, May 17, 2012

PATRICK MAFISANGO OF SIMBA SC IS DEAD

Marehemu Patrick Mafisango (kwenye kiduara) katika picha ya pamoja na kikosi cha Simba enzi za uhai wake.
Mchezaji wa Simba na timu ya Taifa ya Rwanda kiungo mkabaji Patrick Mafisango amefariki dunia kwa ajali ya gari leo alfajiri katika eneo la Tazara jijini Dar es salaam.
Hili ndilo Gari alilopatanalo ajali marehemu Patrick Mafisango maeneo ya TAZARA jijini Dar.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Simba bwana Aden Rage amesema kuwa taarifa za awali juu ya chanzo cha kifo cha mchezaji huyo zinasema kuwa mchezaji huyo amekutwa na mauti akiwa anaendesha gari na kujaribu kumkwepa mwendesha pikipiki.

Msiba huu unakuja wakati kocha wa timu ya Taifa ya Rwanda Milutin Sredovic 'Micho' akiwa amemteuwa kepteni wa zamani wa timu hiyo Hamada Ndikumana a.k.a 'Katauti' na Patrick Mafisango kujiunga na timu ya taifa hilo (AMAVUBI) kwaajili ya maandalizi ya nchi zitakazofuzu kwenda Brazil kwenye michuano ya Kombe la dunia 2014.

Kabla ya  kuichezea Simba mchezaji huyo alitokea Azam Fc ya jijini Dar es salaam.
Patrick Mafisango is dead.
Mwenyezi Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya marehemu Patrick Mafisango.