Sunday, December 16, 2012

SHOW YA KOFFI JIJINI MWANZA


Koffi olomide akitambuklisha kwa mashabiki wake mmoja kati ya wasanii wa nyumbani aliyemvutia Mwanadada Recho toka THT.
Koffi Olomide akiliongoza skwadi lake la madensa jukwaani,full kujiachia.

Pichani shoto ni msanii kutoka THT,Rachel akionesha umahiri wake wa kucheza lingala huku Koffi Olomide akidekshia kwa mbaali hivi,palikuwa hapatoshi watu wangu.

Mwimbaji nyota wa Koffi Olomide,Cindy nae akionesha umahiri wake wa kujimwaya mwaya jukwaa,huku mashabiki (hawapo pichani) wakipiga miluzi na mayowe.

Wadau nao wakijichukulia taswira zao kwa ajili ya kumbukumbu.






Wakazi wa Mwanza walipfika kwenye uwanja wa ccm-kirumba walijionea vilivyo kwamba Koffi Olomide na kundi lake zima la Quartie Latin bado ni moto wa kuotea mbali.

Burudani ikiendelea jukwaani.

Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya SBL,Ephraim Mafuru, Anitha Msangi Maurice Njowoka na Patrick Kisaka kutoka kampuni ya bia ya Serengeti wakiwa katika picha ya pamoa usiku huu ndani ya uwanja wa CCM-Kirumba.

Sehemu ya wakazi wa Mwanza wakifuatilia kwa makini burudani.

Lwaaaaa....!! 

Msanii mahiri kutoka THT,Rachael kama kawaida nyonga yake laiiini inayosisimua mashabiki wake kila awapo jukwaani,na ndivyo kwa wakazi wa Mwanza walivyobaki kupiga mayowe ya shangwe usiku huu ndani ya CCM-Kirumba.

Ilikuwa ni burudani mwanzo mwisho.

Madansa wa Koffi Olomide wakipanda jukwaani kwa staili ya kipekee kabisa tayari kuangusha bonge la burudani kwa washabiki na wapenzi wa kundi la Quartie Latin.

Cindu mwanamuziki mwenye sauti nyororo.laini na safi kabisa akiimba jukwaani kwa umahiri mkubwa huku akipambwa na madensa wa bendi hiyo ya Quartie Latin.

Cindy akiimba kwa hisia jukwaani.

Back up ya ukweli ya Koffi Olomide akiimba kwa pamoja jukwaani.

Mwanamuziki mahiri wa Koffi Olomide,Cindy akipewa maiki mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa CCM-Kirumba usiku huu tayari kwa kuzikonga nyoyo za mashabiki wa kundi lao.Onesho la Tusker Carnival limeandaliwa na kampuni ya Prime Time Promotioni ikishirikiana kampuni dada ya Clouds Media Group,likidhamiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Tusker Lager "bia bora,marafiki wa kweli".


Mwanamuziki Koffi Olomide sambamba na mwimbaji wake nyota Cindy wakiwasili usiku huu kwenye uwanja wa CCM-Kirumba tayari kwa kuwatumbuiza wakazi wa jiji la Mwanza.

Cindy akiwaza jambo jukwaani kwa utulivu mkubwa.


H baba kama kawaida yake..







Ben, Mussa, Suzy na Crew.
Mwanamuziki Nyota wa kimataifa katika anga ya muziki wa dansi  kutoka  nchini DR-.Kongo Koffi Olomide akiwa ameambatana na mwanamuziki wake mahiri katika uimbaji aitwaye Cindy wakishukua jukwaani mara baada ya kumaliza kutumbuiza usiku huu ndani ya uwanja wa CCM-Kirumba jijini Mwanza,Onesho liitwalo Tusker Carniva lilikuwa limedhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Tusker Lager


Koffi Olomide akiingia kwenye mchuma wake mara baada ya kumaliza onesho lake usiku huu na kufanikiwa kuzikonga nyoyo za mashabiki wake kwa kiasi kikubwa.

TPBC YAWATAKIA WATANZANIA WOTE KHERI YA CHRITSMAS!


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
December 16, 2012

Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) inapenda kuchukua fursa hii adimu kuwatakia Watanzania wote sikuu njema ya Kristmas pamoja mwaka mpya ujao wa 2013. Katika mwaka unaoishia tarehe 31 mwezi huu wa 12, TPBC inapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa wadau wote wa ngumi waliosaidia kwa namna moja au nyingine katika maendeleo ya ngumi za kulipwa Tanzania.

TPBC inatambua wazi mchango wa wadau mbalimbali katika kukuza tasnia ya ngumi za kulipwa Tanzania.

1. MABONDIA

TPBC inapenda kuwashukuru mabondia wote waliojitokeza kugombea mataji yake mwaka 2012 katika uzito mbalimbali. Michango yao kwenye kukuza ngumi za kulipwa ni mkubwa sana hususan katika kukuza ajira na burudani. TPBC inachukua fursa hii kuwapongeza mabingwa wake wote katika mwaka 2012.

Aidha TPBC inependa kuchukua fursa hii kuwashukuru sana mabondia wote wa Kitanzania waliocheza nje ya nchi kwa kuitangaza vyema Tanzania. Mchango wao umeongeza na kukuza Utalii wa Michezo kwa Tanzania kwa kiwango kikubwa.

2. MAPROMOTA (WAKUZAJI), MAMENEJA NA MAKOCHA

TPBC inapenda kuwashukuru mapromota, mameneja na makocha wote waliojitokeza na kusaidia kupromoti mapambano mbalimbali mwaka 2013. Mchango wao ni mkubwa sana katika tasnia ya ngumi za kulipwa na tunazidi kuwaomba waendelee kukuza ngumi za kulipwa kwa manufaa ya taifa na wadau wenyewe.


3. VYOMBO VYA HABARI

Vyombo vya habari vikiwamo magazeti, radio, tv, blogs, tovuti, na vinginevyo vimetoa mchango mkubwa sana kwa TPBC katika kufikia malengo yake katika mwaka 2012. Wakati tukimaliza mwaka huu, tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa vyombo vyote vya habari na wanahabari wenyewe katika kukuza ngumi za kulipwa Tanzania.

4. WADHAMINI

TPBC inatambua kuwa mchango mkubwa wa wadhamini katika kukuza ngumi za kulipwa ni muhimu sana. Hivyo tunatoa shukrani kwa wadhamini mbalimbali ambao walitoa mchango wao katika kipindi kinachoishia mwaka 2012 katika kukuza ngumi za kulipwa Tanzania. Tunapenda kuwaomba wadhamini hao na wengine wengi ambao wanaipenda nchi yao kujitokeza kwa wingi katika kuchangia na kukuza tasnia ya ngumi katika mwaka ujao wa 2013 ili Tanzania iweze kwenda mbali zaidi.

5. VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA:

TPBC inapenda kuvishukuru sana vyombo vya ulinzi na usalama vikiongozwa na jeshi la Polisi katika kutoa ulinzi imara wakati wa mapambano mbalimbali katika mwaka huu unaoishia 2012. Mchango wao umesaidia sana katika kulinda usalama wa wadau wa ngumi pamoja na mabondia wenyewe mwaka huu, tunawaomba wazidi kuendelea kutoa ulinzi hususan wakitimiza malengo ya Polisi jamii.

6. MAMLAKA ZA MIJI:

Tunapenda pia kuwashukuru sana mamlaka za miji katika Halmashauri za Manispaa za miji yote ambayo yalisadia wakati wa mapambano mbalimbali yaliyofanyika mwaka 2012. Tunawaomba wazidi kutoa ushirikiano wao katika kipindi cha mwaka 2013.

7. MSAJILI WA VYAMA WIZARA YA MAMBO YA NDANI

TPBC inapenda kushukuru sana ofisi ya Msajili wa Vyana Wizara ya Mambo ya Ndani kwa msaada na ushirikiano wake katika kuendeleza ngumi za kulipwa Tanzania. Tunatambua mchango wake katika kuendeleza ngumi kupitia usimamizi wa ofisi yake kwa vyama vilivyoandikishwa katika ofisi yake kikiwamo TPBC.

8. KURUGENZI YA MAENDELEO YA MICHEZO

TPBC inapenda kutoa shukrani zake nyingi kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini kwa msaada, ushauri na ushirikiano wake katika kusaidia kufikia malengo yake mwaka huu 2012. Tunaomba ushirikiano huu uzidi kuendelea ili tasnia ya ngumi izidi kukua na kuifanya Tanzanai nchi yenye mabondia wazuri duniani.

9. BARAZA LA MICHEZO LA TAIFA (BMT)

Tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru viongozi na maofisa wa Baraza la Michezo la Taifa kwa mchango wao katika kukuza ngumi za kulipwa Tanzania. BMT walitoa misaada yote ambayo TPBC iliomba katika mwaka huu na tunaomba ushirikiano wetu uzidi kuendelea mwaka 2013.


10. WADAU WENGINE WOTE

TPBC inapenda kutoa shukrani zake kwa wadau wote ambao hawakutajwa hapo juu lakini walitoa michango wao katika kukuza ngumi za kulipwa nchini. Tunaenzi sana michengo yenu mungu awabariki.

11. MIPANGO YA MWAKA 2013

TPBC ina mipango kadhaa katika mwaka ujao wa 2013 ikiwamo pamoja na:

1. Kukuza ushirikiano wa karibu na mashirikisho mbalimbali ya michezo ndani na nje ya nchi ili kukuza tasnai ya nguni za kulipwa Tanzania na nje ya nchi kwa manufaa ya mabondia wa kitanzania.
2. Kufanya uchaguzi wake katika mikoa yote na baadaye taifa kuanzia March 2013
3. Kuidhinisha mapambamo mbalimbali ya ubingwa wa mikoa, kanda, taifa na kimataifa
4. Kufanya semina ya maofisa wa ulingo, mapromota, mameneja pamoja na makocha
5. Kuwatafutia mabondai wa kitanzanai ubingwa mbalimbali nje ikiwa ni pamoja na mataji mapya ya Jumuiya ya Madoka kwa bara la Afrika
6. Kuhamasisha watanzania wengi waweze kuwa mapromota (wakuzaji)
7. Kuwahamasisha wadhamini wengi ili kudhamini ngumi za kulipwa
8. Kushirikiana na mapromota na kuwaalika mabondia maarufu duniani kuzuru Tanzania ili kujenga heshima ya ngumi na kuitangaza nchi.
9. Kukuza na kuchangia sekta ya Utalii wa Michezo kwa kuwatumia mabondia wa Kitanzania watakaopigana nje ya nchi kuitangaza vyema Tanzania.

Tunapenda kusema tena:

Watanzania, Kheri ya Kristmas na mwaka mpya 2013.

Merry Xmas and Happy New Year 2013 Tanzanians,

Imetolewa na:


Onesmo A.M.Ngowi
President, Tanzania Professional Boxing Commission (TPBC)
Registered as Societies (Application for Registration) Rules 5, 1954, by United Republic of TANZANIA
Technology House, 35-38 Ghalla Road,
P.O BOX 1106, Moshi - Tanzania
Cell: + 255-754-360828

Saturday, December 15, 2012

MAANDALIZI YA PAMBANO LA CHEKA NA MMLAWI CHIMWEMWE YAKAMILIKA



MAANDALIZI la pambano la Francis Cheka na bondia Chiotka Chimwemwe toka Malawi litakalochezwa Desemba 26 mwaka huu kwenye uwanja wa Sheikh Abeid Amani Karume jijini Arusha yamekamilika.

Akizungumza  jijini Dar es Salaam promota wa pambano hilo Andrew George amesema taratibu za mchezo huo umekamilika.

"Taratibu zote za pambano zimekamilika kwa asilimia 90 ikiwa pamoja na kumtumia tiketi bondia Chiotka Chimwemwe", alisema George.

George alisema ameamua kulipeka pambano hilo Arusha kwa kuwa anaamini watu wa Arusha wanapenda ngumi na siku hiyo ni siku ya sikukuu hivyo watakuja kwa wingi pamoja na familia zao kwani pambano litaanza saa nane mchana.

Pia alisema mabondia watapima uzito siku ya sikukuu ya krismasi jijini Arusha.

Pambano hili litakuwa ni la raundi 12 na Mmalawi huyu anajigamba atampiga Cheka ndani ya ardhi ya nchi yake hivyo kuwasihi watanzania kuja kwa wingi kwani hata ulinzi utakuwepo wa kutosha, alisema George 


MOJA YA MABANGO YALIYOTAPAKAA JIJINI ARUSHA KWA SASA KUHUSU MPAMBANO HUO

NI MATAYARISHO YA LEO KUELEKEA SHOW YA KESHO YA MTU MZIMA KOFFI OLOMIDE MWANZA

Mnyama Dugu moja na wadhamini wetu wa show ya Koffi Olomide nchini Tanzania.


Ikiwa leo mpango mzima unasanukishwa ndani ya jiji la Dar upande wa pili lazima kuhakiki ubora wa stage la Mwanza uwanja wa tukio CCM Kirumba mahala ambapo itamwagwa show ya mtu mzima Koffi Olomide hiyo kesho.


Sound injinia wa Prime times Promotion Dee akifanya 'kalukulesheni' ndani ya dimba la CCM Kirumba jioni ya leo.


Muziki, lights na vimbanga vyose....


Mzigo..mpango

Ndani ya radio washirika Passion Fm 91.0 Mwanza mtangazaji Philbert Kabago akiwa na H. Baba na Ua lake pamoja na vijana wawili 'Hatari' katika dance.


Wapo Rock City ahadi kujumuika na wakazi wa Mwanza kushuhudia makali ya kesho jumapili CCM Kirumba na Mopao'

Sunday, November 4, 2012

BRIGITER ALFRED ANYAKUA TAJI LA REDDS MISS TANZANIA 2012



Taji la Redds Miss Tanzania 2012, limekwenda Kinondoni kwa mrembo toka Sinza aitwaye Brighter Alfred katika tukio lililofanyika jana usiku katika ukumbi wa Uguno Plaza jijini Dar es salaam.

Mshindi wa Taji la Redds Miss Tanzania 2012, Brighter Alfred (katikati) akipunga mkono kwa furaha katika picha ya pamoja na mshindi wa Pili, Eugene Fabian (kushoto) na Mshindi wa Tatu, Edda Sylvester mara baada ya warembo hao kutangazwa kuwa washindi wa shindano hilo. Brigitte anatokea Kitongoji cha Sinza na Kanda ya Kinondoni wakati, Eugene anatoka Mkoa wa Mara na Kanda ya Ziwa huku Edda ni Miss Kigamboni na Kanda ya Temeke.

Warembo waliofanikiwa kuingia hatu5 bora ya Redds Miss Tanzania 2012, kutoka kushoto ni Brigitte Alfred, Eugen Fabian, Happyness Daniel, Edda Sylvester na Magdalene Roy wakipozi kwa picha.

Wageni mbalimbali na wadau wa tasnia ya Urembo nchini Tanzania wakifuatilia shindano hilo kwa umakini ndani ya Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

Wasanii wa kundi la Ngoma za Asili la Wanne Stars likitoa burudani.

Balozi wa Tanga Beach Resort, Happyness Rweyemamu akijinadi jukwaani na vazi lake la ubunifu.

Mshiriki Flavian Maeda kutoka Kitongoji cha Kurasini na Kanda ya Temeke jijini Dar es Salaam akipozi jukwaani na vazi la ubunifu.

Fina Recatus akipita jukwaani na vazi la ubunifu. Fina ni Balozi wa Tanga Beach Resort 2012.

Naomi Jones nae akipita jukwaani na vazi la ubunifu

Mrembo wa Dar Indian Ocean na Kinondoni, Kudra Lupato akikatiza jukwaani.

PICHA NA www.kajunason.blogspot.com

Monday, October 15, 2012

PRIMETIMES PROMOTIONS WAWAPONGEZA WADHAMINI SERENGETI FIESTA 2012

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa shukurani kwa Wadhamini wakuu waliofanikisha Serengeti Fiesta 2012 kufanyika na kumalizika kwa amani kwa mikoa takribani 12 nchini Tanzania ile hali tamasha hilo likiacha alama ya maendeleo na chembe za changamoto ya ukuzaji uchumi kwa wananchi wa mikoa iliyo kuwa kwenye ratiba. 

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa Cheti cha Ushiriki bora kwa wadhamini wa mafuta vyombo vya barabarani GAPCO walioshiriki vyema Tamasha la Serengeti Fiesta 2012. 

Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akitoa Cheti cha Ushiriki Bora kwa wadhamini wakuu Kampuni ya bia SBL kupitia kinywaji mahsusi Tamasha la Serengeti Fiesta 2012, Serengeti Premium Lager walioshiriki vyema kufanikisha mpango mzima mwanzo mwisho. 

Kisha zikafuata shukurani za dhati kutoka kwa Mdhamini mkuu zilizotolewa na Mkurugenzi wa Masoko bia ya Serengeti Ephaim Mafuru.

Msanii mahiri mwenye mbwembwe za kila aina Juma Nature akimwimbia Mtangazaji wa kipindi cha Jahazi Wasiwasi Mwabulambo 'aaaah ... naye alicheza siutani' 

Top in Dar, You can call him TID naye alipata fursa kutoa shukurani zake katika usiku huo maalum wa marafiki kukutana ndani ya Escape Two.

Kwa upande wa msanii wa muziki wa kizazi kipya Shettah amesema kuwa ujio wa tamasha hilo mwaka huu 2012 umetumika kuijenga sanaa yake sambamba na kumweka karibu na mashabiki wake ana uhakika kupata mialiko mingi ya kutosha kwani amekwisha jitangaza vya kutosha naye amejipanga kufanya show levo za kimataifa. 

Mwana FA kwa upande wake amesema hii ni miaka yake ya kusherehekea mafanikio kwa sanaa yake kushika hatamu akimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumtunuku karama ya ubunifu wa mashairi, nyimbo za kueleweka pamoja na umiliki bora wa jukwaa na hadhira.

Tajiri wa Sauti aka Rich Mavoko na shukurani zake ndani ya Part Maalum la Shukurani lililoandaliwa na Primetimes Promotion kuwapongeza wadhamini wa Serengeti Fiesta 2012 nakufanyika Club Escape Two jijini Dar es salaam.

Hip hop thing'

Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania toka kundi la Vuvuzela Entertainment,  Bukuku (katikati) akiwa na wadau.

The Crew.

Watu waliunyuka.....

Wawo....

Men....

Ni Dr. Isaack, Fid Q na mie.

Ze Crew...

Shine....
  
Producer wa Clouds Tv Mr. Mebb.

Dj Mayanga on the one and two.

Fun moment ni Madee, Chege, Morgan na Wasiwasi.
Good.

Wanyama....

Inshort kila kitu kili shine usiku wa jana...
Shukurani kwa Primetimes Promotion kwa kutukutanisha,
Serengeti Premium Lager, GAPCO, PEPSI na Precission Air kwa udhamini.