Tuesday, May 22, 2012

BOB JUNIOR KUPAMBA MISS ILEMELA 25/05/2012 IJUMAA GOLD CREST HOTEL ILE MWaaa!!!



Producer Mkali, Rais wa wasafi mwenye kipaji cha uanamitindo, mwenye mvuto kwa mabinti, mwimbaji mwenye uwezo wa kuichezea sauti yake atakavyo, msanii ambaye tangu kuzaliwa kwake hajawahi kutengeneza video mbovu, msanii mwenye vipaji vingi kuliko wote, Rais wa Masharobaro Bob Junior ndiye atakaye tumbuiza katika Miss Ilemela 2012 .

Miss Ilemela itafanyika Ijumaa hii ya tarehe 25/05/2012 katika ukumbi wa Gold Crest jijini Mwanza. Kiingilio Miss Ilemela 2012 ni shilingi 20,000/= vitikawaida na VIP ambako kutakuwa na sapraiz kibao ni shilingi 40,000/= tu...
Akizungumzia juu ya sifa za wanyange wa Miss Ilemela mratibu wa kinyang'anyiri hicho Bi Ester Morris amesema kuwa warembo wa safari hii wanamvuto na sifa za kuwania taji loloteulimwenguni kwani ilifika wakati aliamua kubadilisha kambi na kutobainisha wapi ameweka kambi rasmi kwa warembowake kwa nia ya kuepuka usumbufu wa kutembelewa mara kwa mara na wadau wasiopitwa na vyenye mvuto.

Sambamba na burudani ya Bob Junior kinyang'anyiro hicho kitapambwa na onyesho la mavazi ya harusi, ufukweni, ofisini na mitoko mbalimbali yakionyeshwa na wadau spesheli. Wadhamini wa miss Ilemela mwaka 2012 ni Sahara Communication, Gold Crest Hotel, Lakairo Investment, Nyanza Bottling Co. LTD, Star Max Electronics, Dunia ya warembo na  G. Sengo Blog.

No comments:

Post a Comment