Tuesday, June 14, 2011

HATIMAYE MOYO WANGU YA PHILBERT KABAGO YATINGA SOKONI!!!

Kabago.
Mkali wa michano kutoka The Rock City Mwanza, ambaye vilevile ni prizenta wa Passion Fm, Philbert Kabago ameshusha rasmi mtaani kitu cha album. Blogu hii imefanikiwa kuchonga na mshtaa' na hiki ndicho alichosema- "Album imetoka rasmi, so na hii ni baada ya kuwa katika maandalizi makubwa, nimeamua kuiachia album hii yenye jina 'Moyo wangu' ikiwa na ngoma kibao za ukweli kama vile 'Dear', 'Moyo wangu' ambayo imebeba jina la album, 'mama' alioimba kumuenzi marehemu mama yake, wivu, 'Umeme wa mgao' ambayo ndio inayotamba kwa sasa kwenye baadhi ya vituo vya radio n.k"

Dj Ali D akishusha mibaraka kwa album.
Kuhusu wasanii aliowashirikisha katika album hiyo jamaa amefunguka kwa kusema kuwa ni pamoja na Farida, MB Dog, Mr hill, Hussein machozi, G.Sengo na wengine wengi. Album imefanyika katika studio mbalimbali zikiwemo Tetemesha Records, Mo Record za mwanza na Family studio Arusha! Wasambazaji ni GMC.

No comments:

Post a Comment